Sunday, November 2, 2014

UJUMBE MAALUMU KWA KIDATO CHA NNE KESHO 03/11/ 2014 JUMATATU

 
KABLA   YA   MTIHANI
{1}.Usiku  unaofuatiwa  na  siku  ya   mtihani  uwe   na  muda  wa  kutosha wa  kulala. Usisome  hadi  usiku  wa  manane. LALA  MAPEMA  SAA  4  USIKU  NA  AMKA  SAA  11  ALFAJIRI.Utakuwa  umelala  SAA  8  kiafya  ni  nzuri . KUMBUKUMBU  YA  MASOMO  itakuwa  vizuri /  Active.
{2}. Siku  ya   Mtihani, Usifikirie  KUSHINDWA  bali  UWE  na   IMANI  kuwa  UTASHINDA. ONDOA   Wasiwasi  na   Mashaka.WAZA  KUFAULU  SIYO  KUFELI.
{3}.Wahi  kwenye   Chumba  Cha  Mtihani  Kwani  Kuchelewa  huleta  HOFU.
{4}. CHUKUA  Vifaa  vyote  muhimu  katika  mtihani  kama  vile  KALAMU, PENSELI,  na   RULA.
{5}.SOMA  RATIBA  YA  MITIHANI  angalia  MASOMO   yako   na   ZINGATIA  MUDA, MUHIMU KULIKO  VYOTE .
{6}.JIKUMBUSHE  KILA  WAKATI   KUHUSU  SHERIA   ZA  MITIHANI.
{&}.Kama   una   TATIZO  LA  KIAFYA hakikisha   Msimamizi  wako    ANAFAHAMU. Mweleze   Mapema.
{7}.JIFARIJI  ,angalia   huku  na  kule    Kuna   Wenzako  pia    kama  wewe   WANAFANYA  MTIHANI PIA. Uwepo  wa  Wenzako  utakufanya   uweze   KUJIAMINI.
{8}. ACHA  KUTAFUTA  FEKI  YA  MTIHANI  UTAFELI  VIBAYA   SANA.

              NDANI  YA   CHUMBA    CHA  MTIHANI

{6}.FANYA   SALA  FUPI  kimoyomoyo  Kumwomba  MUNGU  akuondoe  HOFU/ FEAR  COMPLEX  NA  MASHAKA. OMBEA  WENZAKO  PIA.JIAMINI  NA   UTASHINDA.
{7}.JAZA   NAMBA  YAKO  YA  MTIHANI  na   Maelezo   Mengine MUHIMU  katika   Karatasi   ya  kujibia.
{8}.SOMA   MAAGIZO/ MAELEKEZO  YA  MTIHANI  Kwa   Uangalifu  sana   na  hakikisha  uko  makini  kwa  kile   unachotakiwa  Kufanya  kabla   ya   KUJIBU  SWALI  LOLOTE.
{9}.Kabla  ya  Kujibu   Maswali  ya   Mtihani   ANGALIA   MTIHANI  WOTE.
{10}.Kabla   hujaanza  kujibu  MASWALI , ANGALIA  MASWALI  ambayo  ni  rahisi  kwako  kujibu.
{11}.JIBU   MASWALI  RAHISI  KWANZA  na  kwa   haraka  ili  upate  MUDA  wa  kutosha  KUJIBU  Maswali  Magumu.
{12}.Usijibu  Swali  bila  kuelewa  linataka  nini ? JIBU  utakalojibu  litakuwa  tofauti  na  swali.
{13}. Kama   ni   Swali  la  INSHA   orodhesha   dondoo  utakazotumia  kujibia  swali  husika.
{14}. USIPOTEZE   MUDA  KUNAKILI  SWALI  TENA. Andika   Namba  ya   swali  na   jibu   lake.
{15}.Usiwe  na   haraka  ya   Kumaliza  mtihani   kutakufanya  Usijibu  kwa   makini.
{16}.KUWA   NA  SAA  ya  KUANGALIA  MUDA   Utakavyotumika  wakati   wa   Kufanya  Mitihani
{17}.Acha   Nafasi   kila   baada  ya  SWALI  kwa   ajili   ya   Kuongeza   nukuu   zingine   zitakazojitokeza   baadaye  wakati  wa   Kujibu   Mtihani.
{18}.  Kama  MUDA  umekwisha  halafu   bado   unatakiwa   kujibu   Maswali   Mawili  au   zaidi.  JIBU  KWA  UFUPI  kwa  kila   swali { OUTLINE  ANSWERS }
{19}.Hakikisha  unajibu   swali   sahihi   bila  kukosea  namba  ya  swali. ANGALIA  USICHANGANYE   NAMBA  YA   SWALI. UTAKOSA   MAKSI  KWA  KUJIBU  SWALI  AMBALO  SIYO  SAHIHI. 
{20}. Tenga  MUDA  KIDOGO  WA  KUPITIA  MTIHANI  WAKO  WOTE  MASWALI   PAMOJA  NA  MAJIBU  YAKE.
{21}.Kila   baada   ya   Kumaliza   Mtihani   USIPENDE  KUJADILIANA  MAJIBU  YA  MTIHANI  WAKO  PAMOJA   NA  MARAFIKI  ZAKO. Itakufanya   Ujenge  HOFU   na  WASIWASI  pindi  utakapogundua   umekosa   swali.  JIFUNZE  KUSAHAU   MTIHANI  uliotoka  Kufanya.  ANGALIA  Mitihani  Inayokuja.
{22}.GAWA  MUDA  WAKO  VIZURI.Angalia  Idadi   ya   MASWALI   Unayotakiwa  Kujibu  Na   Jumla  ya   Muda wa   Kumaliza   Mtihani  HUSIKA.
{23}.  Hakikisha  Unapanga  Mtihani  wako  katika   Mpangilio   Mzuri    Maswali   na  Majibu.


                       "MAY   YOU   BE    SUCCESSFUL"  

No comments:

Post a Comment