Wednesday, March 25, 2020

MWONGOZO WA KUFANYIA KAZI AU KUJISOMEA KWA WANAFUNZI NYUMBANI !!

FAIDA  ZA  KUFANYIA  KAZI  / KUJISOMEA  NYUMBANI.
Kufanyia kazi zako nyumbani, iwe umeajiriwa au umejiajiri au  wewe  ni  mwanafunzi wa  shule  za   msingi , sekondari  au  chuo   kuna faida nyingi sana, baadhi ya faida hizo ni kama ifuatavyo;
  1. Unaokoa muda mwingi ambao huwa unaupoteza kwa kwenda eneo la kazi, shule au  chuo  Kuanzia muda unaotumia kwenda, kurudi na mwingine unaopotea, kwa kufanyia kazi nyumbani hupotezi muda wako.
  2. Unapunguza fursa za kupoteza muda zinazopatikana kwenye eneo la kazi, mfano mikutano mbalimbali ambayo hufanyika maeneo ya kazi, ambayo kwa sehemu kubwa haina tija.
  3. Unafanya kazi kwa mpango wako bila ya kusumbuliwa na wafanyakazi wengine.Kama  mwanafunzi  au  mwanachuo unaepuka  kelele  za  wanafunzi  wenzako . Japo kunakuwa na mawasiliano ya simu au njia nyingine za mtandao, ile hali ya kukatishwa na wengine wakati unafanya kazi  au  unajisomea  inapungua.
  4. Kwa sehemu kubwa unakuwa na uhuru wa kupanga muda wako mwenyewe, hasa kama kazi yako haihitaji kushirikiana na wengine wakati mnaifanya. Unaweza kupanga kufanya kwa muda unaofaa kwako.
  5. Unapata muda mwingi wa kupumzika, majukumu yako unayofanya ukiwa kazini, shule , chuo ukiyafanyia nyumbani itakuchukua nusu ya muda unaotumia kuyafanya ukiwa kazini , shule  au  chuo .Hivyo unapata muda mwingi wa kupumzika au kufanya mambo mengine.
Changamoto za kufanyia kazi nyumbani.
Hakuna kisichokuwa na changamoto, na katika kufanyia kazi nyumbani, zipo changamoto nyingi. Hapa ni baadhi ya changamoto hizo;
  1. Kushindwa kutekeleza majukumu yako kwa wakati kwa sababu hakuna anayekusimamia moja kwa moja au anayekuangalia. Unahitaji nidhamu kali sana kuweza kujisimamia mwenyewe.
  2. Usumbufu wa wanafamilia wakati unafanya kazi, wengi hawajui kwamba japo upo nyumbani pia upo kazini, hivyo kuingilia kazi zako pale wanapokuwa na mahitaji mbalimbali.
  3. Kukosekana kwa mipaka kati ya kazi na maisha. Kwa kuwa unafanyia vyote nyumbani, ni rahisi kushindwa kuweka mipaka, ukajikuta unaruhusu mambo ya kifamilia kuingia kwenye wakati wa kazi au mambo ya kikazi kuingia kwenye wakati wa familia.
  4. Wageni usiokuwa na miadi nao wanapokuja nyumbani na kujua upo, wanaingilia sana muda wako wa kazi. Wengi hawawezi kuelewa kwamba japokuwa upo nyumbani, upo kazini, hivyo kuhitaji muda wako mwingi.
  5. Ni rahisi kwa uvivu kukunyemelea, ukipatwa na usingizi kidogo ni rahisi kwenda kulala au kufanya mambo mengine ya kupoteza muda kama kuangalia tv, kuzurura mitandaoni na kadhalika.
MKAKATI  BORA  KWAKO  WA   KUFANYIA  KAZI  NYUMBANI.
Ili kupata manufaa ya kufanyia kazi nyumbani, pamoja na kuzuia changamoto zake zisiwe kikwazo kwako, tengeneza mkakati mzuri kwako kufanyia kazi nyumbani
Zingatia mambo yafuatayo katika kutengeneza mkakati wako wa kufanyia kazi nyumbani utakaokupa matokeo mazuri.
( 01 ). TENGA  ENEO  LA  KUFANYIA  KAZI.
Kitu cha kwanza muhimu kabisa kwako kufanya ni kutenga eneo la kufanyia kazi ukiwa nyumbani. Huwezi kuwa unafanyia kazi kila mahali na ukawa na nidhamu nzuri. Badala yake unapaswa kutenga eneo ambalo utakuwa unafanyia kazi zako, na ukiwa eneo hilo unachofanya ni kazi tu na siyo kitu kingine.
Hii inakuandaa kisaikolojia kuheshimu eneo hilo na unapokuwa kwenye eneo hilo unajua cha kufanya ni kazi. Kama unaishi kwenye nyumba kubwa unaweza kutenga chumba utakachotumia kama ofisi. Lakini kama huwezi kufanya hivyo unaweza kutenga eneo kwenye chumba chochote, hata kile unacholala na kulitumia kama eneo la kazi.
Kama unatenga eneo ndani ya chumba chenye matumizi mengine, hakikisha unaweka kiti na meza kwa ajili ya kufanyia kazi. Hivyo unapokaa kwenye kiti na meza hiyo, unajua kabisa hili ni eneo la kazi. Usifanye kitu kingine unapokuwa kwenye kiti na meza ulivyoandaa kwa ajili ya kazi.
Epuka kufanyia kazi kitandani au kwenye kochi, kwenye maeneo hayo hutaipa kazi uzito kwa sababu kisaikolojia unayachukulia kama maeneo ya kupumzika
 ( 02 ). TENGENEZA  RATIBA  YAKO  YA  KILA  SIKU  NA  IFUATE.
Japokuwa una uhuru wa muda gani ufanye kazi unapokuwa nyumbani, uhuru huo una mipaka. Huwezi kufanya kazi zako pale unapojisikia, ukienda kwa mpango huo hutafanya chochote. Ndiyo una uhuru, lakini lazima utengeneze ratiba yako mwenyewe na uifuate kila siku.
Panga kabisa ni muda gani unaamka, ukiamka unafanya nini, muda gani unapumzika, unakula na unakuwa na familia. Yote hayo lazima uyapange na kisha kuyafuata.
Ukianza siku zako bila mpango, utajikuta umefanya mengi, umechoka lakini hakuna kikubwa ulichokamilisha.
Kwenye ratiba yako ya siku tenga kabisa masaa ambayo huhitaji usumbufu, hayo ni masaa ya kazi zinazohitaji umakini mkubwa.
( 03 ). VAA  KAMA  UNAENDA  KAZINI / SHULENI / CHUONI
Unapofanyia kazi nyumbani, una uhuru wa kuvaa utakavyo au hata kutokuvaa kabisa. Lakini hilo unapaswa kuwa nalo makini, kwa sababu lina madhara ya kisaikolojia kwenye utekelezaji wa majukumu yako ya kazi. Kama umevaa nguo za kawaida utajiona kama hauna majukumu makubwa.
Hivyo unapaswa kujiandaa vizuri kama vile unaenda kazini  shuleni, chuoni kwa kuvaa kabisa nguo zako za kazi na kisha kukaa eneo lako la kazi wakati unafanya kazi. Unapovaa nguo kama vile unaenda kazini, akili yako inakupa uzito wa kikazi na unatekeleza majukumu yako vizuri. 
( 04 ). WATU  WOTE  WAJUE  RATIBA  YAKO.
Ukishaweka ratiba yako ya siku, kila mtu kwenye familia anapaswa kuijua. Na waeleze wazi kwamba japokuwa upo nyumbani, lakini pia upo kazini au  unajisomea. Kwa muda ule wa kazi, mambo yote hapo nyumbani yanapaswa kuendelea kama vile wewe haupo kabisa.
Ule muda ambao umetenga usisumbuliwe, usisumbuliwe kweli, labda kwa jambo la dharura, ambalo hata kama ungekuwa kazini basi ungepigiwa simu. Na weka kabisa vigezo vya dharura ni vipi. Usipofanya hivi, watu watatumia uwepo wako kuuliza vitu mbalimbali na hilo kuathiri kazi zako.
Kuhusu wageni, kama kuna mgeni amekuja na hukuwa na miadi naye, usikutane naye wakati ambao unafanya kazi. Anapaswa kuelezwa ratiba yako na muda mzuri kwako kukutana naye. Na kama ni mgeni muhimu, unaweza kumsalimia na kumpa ratiba yako ilivyo na mkapanga muda gani mzuri wa kuwa na maongezi, kama yapo na ni muhimu.
( 05 ). TENGENEZA  MIPAKA YA  KAZI / KUSOMA  NA  MAISHA.
Kwa kuwa upo nyumbani na unafanyia kazi nyumbani, mpaka kati ya kazi na maisha unafutika kabisa. Wakati wa kazi utaingiliwa na mambo ya kifamilia na wakati wa familia utaingiliwa na mambo ya kikazi.
Ni lazima utengeneze mpaka kati ya kazi na maisha, ufanye kazi wakati wa kazi na maisha wakati wa maisha. Jisukume kutekeleza majukumu yako ya kazi kwa wakati uliopanga kufanya kazi na ule wakati uliopanga kupumzika au kuwa na familia basi usiruhusu kazi au  masomo kuingilia wakati huo.
( 06 ). TUMIA  VIFAA  VYA  KUONDOA  USUMBUFU.
Kama mazingira ya nyumbani kwako siyo rafiki kwako kupata utulivu wa kazi au kusoma, labda kuna kelele mbalimbali za majirani na watu wengine, basi tumia vifaa vya kuondoa usumbufu.
Hapa unapaswa kuwa na spika za masikioni (headphone au earphone) ambazo utazivaa wakati wa kufanya kazi. Kuna ambazo zina sifa ya kufunga kelele za nje zisikuingie na hivyo kukupa utulivu mkubwa wa kufanya kazi zako.
Pia kitendo cha kuvaa spika hizo, kinamfanya mtu asikusemeshe mara kwa mara, kwa sababu anajua humsikii. Pia mtu anapokusemesha, jifanye kama humsikii, hata kama unamsikia, hasa pale jambo linapokuwa siyo muhimu.
Inayoendana na hii ni kuandaa orodha ya nyimbo (playlist) zinazokupa utulivu na kuitumia wakati unafanya kazi zako. Hapa unasikiliza nyimbo hizo kwa kujirudia rudia na hilo linafanya akili yako izame kwenye kazi unayofanya na kuepuka usumbufu.
( 07 ). JALI  AFYA  YAKO.
Unapofanyia kazi nyumbani, kama kazi zako ni za kutumia akili na unazipenda sana, unaweza kujikuta umekaa kwenye kazi siku nzima na hujatoka kabisa nje ya nyumba yako. Pia ulaji ni rahisi sana unapokuwa nyumbani kuliko ukiwa kazini, ni rahisi kula mara kwa mara ukiwa nyumbani kuliko ukiwa kazini.
Hivyo unapaswa kuwa na mkakati wa kujali na kuboresha afya yako. Kitu cha kwanza muhimu ni kufanya mazoezi, tenga muda wa kufanya mazoezi ambayo yatakutoa jasho. Cha pili ni kudhibiti ulaji, usile kwa sababu kuna kitu cha kula, bali kula kwa utaratibu maalumu na kuwa makini na kile unachokula. Cha tatu ni muda wa kupumzika, unaweza ukakosa mapumziko mazuri japo uko nyumbani na hilo likaathiri afya yako.
(08 ). PANGILIA  MUDA  UNAOENDANA  NA  WEWE  NA  UNAOEPUKA  USUMBUFU.
Kitu kimoja ambacho kimekuwa kinanisaidia sana mimi binafsi kuweza kukamilisha sehemu kubwa ya uandishi ni kutenga muda wa uandishi ambao unaendana na mimi na pia unaepuka usumbufu.
Huwa ninaamka saa kumi kamili asubuhi kila siku na baada ya kufanya tahajudi na tafakari kisha kuipangilia siku, kuanzia saa kumi na nusu mpaka saa 12 kamili huo ni muda wa kuandika tu, sifanyi kingine kwenye muda huo. Kwa muda huo, nimekuwa na uwezo wa kuandika kwa kiwango kikubwa sana, kwa sababu akili inakuwa na utulivu na hakuna usumbufu, maana watu wengine wanakuwa wamelala kwenye muda huo.
Hivyo na wewe pangilia majukumu yanayohitaji utulivu na umakini kulingana na wewe binafsi na mazingira. Yaani yapange kwenye muda ambao akili yako iko vizuri lakini pia hakuna usumbufu wa nje.
Watu tumegawanyika kwenye makundi mawili; kuna ambao wanaweza kuamka asubuhi na mapema na akili zao zikawa vizuri (early birds) na kuna ambao wanachelewa kulala na muda wa usiku ndiyo akili zao zinakuwa vizuri (night owls). Jijue wewe uko kundi gani, kisha tenga muda ambao wengine wamelala na ufanye kuwa wa kazi.
Mfano kama uko vizuri kwenye kuamka asubuhi basi amka asubuhi na mapema sana, labda saa tisa au saa kumi na kisha tumia masaa mawili ya kwanza kwenye kazi inayohitaji umakini wako na utulivu. Muda huo wengi wanakuwa wamelala na hivyo usumbufu unakuwa mdogo.
Na kama unachoelewa kulala basi tenga masaa mawili ya usiku mnene ambapo wengine wamelala na akili yako imetulia kufanya kazi.
Ukiweza kutenga masaa mawili ambapo akili yako imetulia na ina umakini na hakuna usumbufu wa nje, kisha kuyaweka masaa hayo mawili kwenye kazi, utatekeleza majukumu makubwa kuliko anayefanya kazi siku nzima kwenye ofisi isiyo na utulivu.
Rafiki yangu mpendwa, mdau  wangu  huu ndiyo mwongozo sahihi kwako wa kufanyia kazi nyumbani .(  kama  wewe  ni  MWAJIRIWA , UMEJIAJIRI , MWANAFUNZI , MWANACHUO  ni  mwongozo  mzuri  sana  kuufuata.

MBINU NA KANUNI ZA KUSOMA NA KUFAULU MITIHANI

UTANGULIZI

Kila mzazi angependelea mwanae afanikiwe katika masomo na kufaulu mitihani yake. Pia kila mwanafunzi anahitaji kufaulu katika mitihani yake. Walimu nao hujisikia vizuri wakati wanafunzi wao wanapofanya vizuri katika mitihani yao. 

Kufaulu mtihani ni muhimu kwa malengo ya mwanafunzi, kwani anaposhinda mitihani humwezesha kuwa na mtazamo wa juu kielimu, kwa mfano kupata cheti, diploma au digrii, kitu ambacho humfanya afae kwenye kazi. Wakati mwingine inakuwa ni viguinu kwa baadhi ya wanafunzi kumudu masomo na mitihani yao. Wakati huohuo wapo baadhi yao ambao wao kufaulu mitihani si tatizo.
Sasa mtu anaweza kujiuliza, kwa nini wanafunzi wengine washindwe na wengine wafaulu vizuri katika masomo na mitihani yao? Mafanikio katika masomo na kufaulu mitihani kunahitaji uwezo wa asili, kufanya kazi kwa bidii na kufuata kanuni na mbinu za kusoma.

Wanafunzi wengine huona ugumu katika masomo na kufaulu mitihani, si kwa sababu hawana akili, bali hawafuati mbinu na kanuni ftilani za kusoma na kufaulu mitihani. Wengi wana uwezo mzuri, kama watajifunza mbinu hizi. Mbinu na kanuni hizi zinaweza kutumiwa na wanafiinzi wa shule za msingi, sekondari, vyuo na hata vyuo vikuu.
Kanuni na   mbinu  za Kusoma ni kama ifuatavyo: 

 JIJENGEE   NIDHAMU BINAFSI  YA  HALI  YA  JUU  YA  KUJISOMEA   KILA  SIKU.

 -----Weka lengo maalum la kusoma kila siku na litimize.
 -----Weka ratiba ya kila somo na ifuate.
-----Tenga muda wa kutosha kwa kila somo.
----- Jiwekee muda wa kutosha kila siku kwa ajili ya kazi za utoaji taarifa za masomo na projekti.

 -----Uwe na mahali maalumu pa kusomea.   
------Epuka kitu chochote kinachoweza kukufanya usisome vizuri.
 ---- Jisomee katika muda unaodhani unataa zaidi.
 -----Uwe na muda wa kupumzika kila unapochoka kusoma.
----- Usifanye mambo mengi kwa wakati mmoja. Kwa mfano, mapenzi au anasa za kimwili wakati ungali mwanafunzi. Hivyo ni vikwazo masomoni.
---- Tafuta mahali pasipo na kelele za aina yoyote.
----- Epuka vishawishi vinavyoweza kukufanya uairishe kujisomea. 

------Fanya mazoezi ya mwili mara kwa mara.



 JIANDAE  MUDA  WOTE SOMA  KILA   WAKATI  NI   MUDA   WA   KUSOMA---USIPOTEZE   MUDA. 
-----Kabla hujaanza kujisomea, hakikisha kuwa zana zote muhimu kwa kusomea zipo.
----- Hakikisha kuwa mahaii pa kusomea pana mwanga wa kutosha.

----- Epuka kusoma ukiwa umejilaza kitandani.
----- Unapokuwa na matatizo kimasomo, mwone mwalimu, anayehusika.
------ Uwe na muda mwingi wa kujisomea kila siku, usipoteze muda kwa mambo yasiyo ya lazima kama vile maongezi.
------ Jiandae kwa mtihani kila wakati, usingoje mwalimu atangaze kuwa ataleta mtihani ndipo usome.
----- Epuka kusoma hadi usiku sana; utaharibu afya yako. 
------ Hudhuria shughuli zote za shule nje ya darasani. 
 
KUWA   KING" ANG"ANIZI , PIGANA , KOMAA , PAMBANA, KUWA   MBISHI---USIKATE   TAMAA   

----Jenga tabia ya uvumilivu na kamwe usikate tamaa wakati ugumu unapoibuka masomoni.
---- Jenga tabia ya kupania kufaulu katika masomo yako.
----- Amini kuwa utafaulu.
-----Epuka kuwaonea wivu na kujilinganisha na wengine kimasomo, bali, jifunze tu siri za mafanikio yao.
-----Chunguza masomo yao ili ujue udhaifti wako uko wapi.

     WAKATI  UNAPOKUWA  SHULENI  , CHUONI   
----Fika darasani kwa wakati unaotakiwa ili usikose maagizo.
----Usikose kipindi bila sababu maalumu.
 ---Wakati mwalimu hajafika darasani, pitia yale uliyojifunza kipindi kilichopita.
----Usisome mambo mengi kwa wakati mmoja.
 ---Soma kazi zako zote za darasani kabla ya kuanza darasa.
 ---Usiwe mtu wa kukaa tu darasani, uliza na jibu maswali yanapoulizwa.
 ---Uwe mwanafunzi mdadisi wa mambo kwa walimu na hata kwa wanafunzi wenzako pia. 

----Wasilisha kazi za darasani kwa wakati wake.
----Baada ya kipindi, pitia yale uliyojifunza.

----Epuka kukaa kimya na nyuma ya darasa, bali shiriki katika mazungumzo ya darasani na wenzako.
---- Jenga uhusiano mzuri kwa walimu wako na kwa wanafunzi wenzako. Ukiwa na amani moyoni, utasoma na kuelewa. Jistahi na kuwapenda walimu wako. Ukimpenda mwalimu utalielewa vizuri somo lake.


JINSI  YA  KUJIFUNZA  LUGHA  YOYOTE  YA   KIGENI--Mfano :-Kiingereza , Kifaransa , Kichina , Kijerumani , n.k  
  
-------Kama unajifunza lugha ya kigeni, Fanya marudio, mazoezi mengi na soma vitabu vingi vya hadithi vya lugha hiyo.-
------ Soma ukiwa na kamusi na tafuta maana ya neno usilolijua.
----- Jizoeze kusikiliza na kuongea ukiwaiga wajuao ujifunzapo lugha ya kigeni.
-----Sikiliza mihadhara na redio ili ujifunze kwa wengine wanavyotamka maneno.
-----  Jikumbushe maneno magumu kila siku.
------ Kila nafasi unayoipata itumie kwa kusoma.
------ Pambana na sarufi za lughaya kigeni kikamilifu.
------ Jifunze lugha ya kigeni kwa kuongea mara kwa mara.
------- Ni jambo la busara kuwa na usiku mmoja wa kupunzika katikajuma ambayo si Jumapili au Jumamosi. 

JIHUSISHE    NA  WENGINE  UNAPOKUWA    MWANAFUNZI(  JIJENGEE  TABIA  NJEMA ) 
----- Ni muhimu kujihusisha na watu wengine, jambo hili litakufariji kimawazo.
-----Ni vizuri pia kuwa na mwanafunzi mwenzio wa kujadili naye.


EPUKA    HAYA  UKIWA   MWANAFUNZI    
-----Epuka marafiki wabaya wenye nia ya kukupotosha.
-----Epuka pombe, uvutaji wa sigara, bangi na madawa ya kulevya. Huharibu ubongo na kudhoofisha afya.
----Jijengee tabia njema ya kujizuia katika tamaa za mwili.

KABLA   YA   MITIHANI  FANYA   HAYA

 ------Kabla ya mtihani, soma kwa bidii sana usingoje mtihani umekaribia ndipo usome.
--------Usiku unaofuatiwa na siku ya mtihani uwe na muda wa kutosha wa kulala. Usisome hadi usiku wa manane.
------  Soma kwa mpangilio kila siku ili kujiandaa kikamilifu kwa mtihani.
--------Siku ya mtihani, usifikirie kushindwa bali uwe na imani kuwa utashinda. Ondoa wasiwasi na mashaka.
------  Wahi kwenye chumba cha mtihani kwani kuchelewa huleta hofu.
------ Chukua vifaa vyote muhimu katika mtihani kama vile kalamu, penseli na rula. 

 UNAPOKUWA   NDANI   CHUMBA   CHA  MTIHANI  FANYA  HAYA
 ----- Soma maagizo ya mtihani kwa uangalifu sana, na hakikisha uko makini kwa kile unachotakiwa kufanya kabla ya kujibu swali lolote. 
-----Kabla hujaanza kujibu maswali, angalia maswali ambayo ni rahisi kwako kujibu..
-----Jibu maswali rahisi kwanza na kwa haraka ili upate muda wa kutosha kujibu maswali magumu.
 ----------------------------------------------------------------------------------
           "USHINDI    NI    WAKO   UNASTAHILI "


TUPO PAMOJA, TUTAKUTANA KILELENI.  SEE   YOU    AT   THE   TOP
 
Ndimi  Rafiki na  Kocha  Wako  Mwl    Japhet  Masatu , Dar  es  salaam ,Tanzania , Afrika   Mashariki , 


Mwl   Japhet   Masatu  ni   Mwalimu  Kitaaluma , Kocha  wa Maisha  na   Mafanikio ,  Mshauri , Mwalimu,  Mjasiriamali , Public  Speaker


 KWA  MAELEKEZO    ZAIDI  TUWASILIANE   KWA



WhatsApp /  Call  / Message + 255 716 924136 / + 255 755 400128 / + 255 688361539

Tuma   MAONI , USHAURI , CHANGAMOTO  KWA  EMAIL :
studentsgotz.9@gmail.com