AN ONLINE PLATFORM THAT PROVIDES EDUCATIONAL CONTENT,SYLLABUSES, STUDY NOTES/ MATERIALS ,PAST PAPERS, QUESTIONS & ANSWERS FOR THE STUDENTS,FORM I--VI ,RESITTERS,QT, ADULT LEARNERS, COLLEGE STUDENTS, PUPILS, TEACHERS, PARENTS,TEACHERS OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA AND WORLDWIDE.YOU ARE WELCOME TO SHARE YOUR KNOWLEDGE AND IDEAS.ENJOY MASATU BLOG.YOU CAN MAKE A DIFFERENCE.YOU CAN ACHIEVE EXCELLENCE. "LEARN.REVISE.DISCUSS".Anytime, Anywhere.
- HOME
- UTAKUZAJE UWEZO WAKO WA LUGHA ?
- MBINU ZA KUSOMA NA KUFAULU MITIHANI
- HOW TO IMPROVE YOUR MEMORY
- ONLINE LEARNING & DISTANCE LEARNING ( E--LEA...
- O-LEVEL & A--LEVEL SYLLABUS
- FORM FOUR ( F 4 )--SUBJECTS---TANZANIA
- FORM TWO ( F 2 )--SUBJECTS---TANZANIA
- FORM ONE ( F 1 )-- SUBJECTS---TANZANIA
- FORM FIVE( F 5 ) AND SIX ( F 6 )--SUBJECTS ---TANZANIA
- FORM THREE ( F 3 ) SUBJECTS----TANZANIA
- STANDARD 1 & 2 SUBJECTS / MASOMO YA DARASA 1 & 2-...
- STANDARD 3 & 4 SUBJECTS / MASOMO YA DARASA 3 & 4...
- STANDARD 5, 6 & 7 SUBJECTS / MASOMO YA DARASA...
Thursday, April 30, 2020
Tuesday, April 28, 2020
Monday, April 27, 2020
FORM TWO ( F 2 )---EXAMS PAPERS--BIOLOGY, PHYSICS, CHEMISTRY, BASIC MATHEMATICS, GEOGRAPHY , HISTORY , KISWAHILI , ENGLISH, CIVICS , ARABIC LANGUAGE , ELIMU YA DINI YA KIISLAMU---MARCH--APRIL , 2020--CORONA HOLIDAY EXAMINATIONS--KINONDONI MUSLIM SECONDARY SCHOOL---DAR ES SALAAM--TANZANIA---- ( PDF )
Sunday, April 26, 2020
Thursday, April 23, 2020
Tuesday, April 21, 2020
Monday, April 20, 2020
Sunday, April 19, 2020
Friday, April 17, 2020
Monday, April 13, 2020
Sunday, April 12, 2020
Saturday, April 11, 2020
Friday, April 10, 2020
Thursday, April 9, 2020
Wednesday, April 8, 2020
Monday, April 6, 2020
UMEZALIWA ILI UFANIKIWE / YOU ARE BORN TO SUCCEED. HUFANIKIWI KWA SABABU ZIFUATAZO : --
 Mambo kumi ( 10 ) unayopenda kufanya kila siku, ambayo yanakuzua isifikie ushindi wako :--
( 1 ). HUJACHAGUA  KUWA  MSHINDI.
Hatua
 ya kwanza kuchukua ili kufikia ushindi kwenye maisha yako, ni kuchagua 
ushindi unaotaka kwenye maisha yako. Upo usemi kwamba kama hujui 
unakokwenda, njia yoyote itakuwa sahihi kwako. Hivi ndivyo wengi 
wanaendesha maisha yao, hawajui wanataka nini, ila wako bize kweli 
kweli.
Chagua leo unataka ushindi wa aina gani kwenye maisha yako ili uweze kuchukua hatua sahihi za kukufikisha kwenye ushindi huo.
 ( 2 ). HUJACHUKUA  JUKUMU  LA  MAISHA  YAKO.
Kama
 umewahi kulalamika au kumlalamikia mtu mwingine juu ya jambo lolote 
linalohusu maisha yako, basi jua unajizuia kushinda. Washindi wanachukua
 jukumu la maisha yao kwa asilimia 100. Chochote kinachotokea kwenye 
maisha yao, wanajua wa kwanza kulaumiwa na kulalamikiwa ni wao wenyewe. 
Kulalamika na kulaumu ni rahisi, lakini inakufanya ujione usiye na hatia
 na uwezo wa kupambana kwenye maisha yako.
Amua leo kushika hatamu ya maisha yako, chukua jukumu la maisha yako kwa asilimia 100 kwa kutokulalamika au kumlaumu yeyote.
(3 ). HUAMINI  KWAMBA  UNAWEZA  KUSHINDA / KUFANIKIWA.
Unapokutana
 na changamoto kidogo, unakata tamaa na kuona safari ya mafanikio 
haiwezekani. Watu wanapokupinga na kukukosoa unawasikiliza na kuona wapo
 sahihi kuliko wewe. Na hilo limekuwa kikwazo kwako. Ushindi unataka 
ujiamini kupitiliza, uamini unaweza kufanya chochote unachopanga, licha 
ya ugumu au changamoto unazopitia. Na ukweli ni kwamba, ukiamini na 
kuamua, hakuna kinachoshindikana.
Jiamini kwamba unaweza kushinda, licha ya magumu na changamoto unazopitia, endelea kuweka juhudi na utafikia ushindi mkubwa. 
( 4 ). HUNA  MALENGO  YANAYOPIMIKA.
Dhana
 yako ya malengo ni potofu, kwa sababu unajiambia tu kwamba mwaka huu 
nitafanikiwa zaidi, nitaongeza kipato, nitaanzisha biashara na 
kadhalika. Kujiambia kauli kama hizo siyo malengo, bali ni matamanio. 
Malengo ni pale unapopanga nini unataka, kwa kiwango gani na kufikia 
lini. Kama umepanga kuanza biashara, unajiambia kabisa ni biashara ya 
aina gani na utakuwa umeianza kufikia tarehe gani. Kama huwezi kupima 
malengo, huwezi kuyafikia.
Weka
 malengo yanayopimika na kila siku jipime kwa malengo hayo, gawa malengo
 hayo kwenye hatua za kuchukua na kila siku chukua hatua hizo bila 
kuacha na utafika kwenye ushindi.
 ( 5 ) . UMEKOSA   UAMINIFU.
Umekuwa
 unasikiliza kauli za wale walioshindwa, ambao wanaamini wale 
waliofanikiwa kuna namna wamefanya. Utawasikia masikini wakisema 
matajiri ni wezi na walaghai. Utawasikia wasioweka juhudi wakisema 
waliofanikiwa wana bahati. Wengine wanakuja kwako na njia za mkato za 
kufanikiwa, ambazo hazihitaji kazi yoyote. Wewe kwa kutokuijua misingi 
ya mafanikio, unaingia kwenye mitego hiyo, kinachotokea ni unajikuta 
unapoteza muda wako na hakuna hatua unazopiga.
Chagua
 kuwa mwaminifu, kufanya kile kilicho sahihi kulingana na misingi ya 
mafanikio na siyo kudanganyika au kufuata mkumbo. Njia zisizo sahihi 
zinaweza kukupa ushindi, lakini hautadumu. 
(6). HUWEKI  KAZI.
Umesikiwa
 watu wanakuambia usifanye kazi kwa nguvu, bali fanya kwa akili, wana 
kiingereza chao wanakuambia Don’t work hard, work smart. Ni uongo, 
hakuna ushindi unaopatikana bila kuweka nguvu na akili, tena kwa viwango
 vya juu sana. Watu wengi ni mashabiki na wafuatiliaji wa michezo 
mbalimbali. Nitajie mchezaji mmoja unayemkubali sana, ambaye wakati 
wenzake wanaenda kwenye mazoezi ya nguvu, yeye anafanya mazoezi kwa 
akili? Hakuna. Halafu wewe unajidanganya kwamba unaweza kufikia ushindi 
kwa akili bila nguvu!
Amua
 kuweka kazi, kazi hasa na siyo ya kitoto. Fanya kazi kwa juhudi na 
maarifa, nenda hatua ya ziada, toa thamani kubwa na ushindi utakuwa 
wako.
(7 ). HUTHAMINI  MUDA  WAKO.
Unauchukulia
 muda wako poa sana, unautawanya kama vile una chemchem ya muda isiyo 
kauka. Unapoteza muda wako wa thamani kwenye mambo yasiyo na mchango 
wowote kwenye ushindi wako, kwa sababu hujui hata thamani ya muda huo. 
Unahangaika na habari mbalimbali, umbeya, udaku, maisha ya wengine na 
mengine mengi. Halafu unakuja kulalamika kwamba huna muda wa kufanya 
zaidi yale uliyopanga kufanya.
Upe
 muda wako thamani, jua ni kiasi gani cha kipato unataka kupata, kisha 
kigawe kwa masaa na jua saa yako moja ina thamani ya shilingi ngapi. 
Hivyo unapopoteza muda, unajua kabisa ni kiasi gani cha pesa umepoteza.
 (8 ). UNASIKILIZA  SANA  HOFU  ZAKO.
Hakuna
 mtu asiyekuwa na hofu, ila wewe unazisikiliza sana hofu zako, hivyo 
huthubutu kufanya kitu chochote kipya na kikubwa, kwa sababu unahofia 
kushindwa. Wanaoshinda wanapata hofu kama zako, lakini wanajua dawa ya 
hofu ni kufanya. Kuwa na hofu ni kawaida, ila kuzisikiliza hofu zako na 
kuzifuata ni kuchagua kuukosa ushindi.
Amua leo kuchukua hatua kwenye yale unayohofia, kwa sababu ndiyo yamebeba mafanikio yako na dawa ya hofu ni kufanya unachohofia.
 ( 9 ). HUJIFUNZI  KILA  SIKU.
Unapata
 muda wakula mara tatu kwa siku, kufuatilia habari, kufuatilia maisha ya
 wengine na kulala, lakini unajiambia huna muda wa kusoma vitabu. Hapo 
ndipo unapoagana na ushindi wako. Kwa sababu hakuna mshindi ambaye 
hajifunzi kila siku. Moja ya mahitaji ya maisha ya ushindi ni kila siku 
kuwa bora kuliko siku iliyopita, na ubora pekee utaupata kupitia 
kujifunza kila siku na kufanyia kazi yale unayojifunza.
Chagua
 sasa kujifunza kila siku, haijalishi siku yako imebana kiasi gani, 
hakikisha unatenga muda wa kujifunza kupitia usomaji wa vitabu na 
mafunzo ya aina nyingine. Usikubali siku ipite hujajifunza kitu kipya.
 ( 10 ). BADALA  YA  KUZALISHA  MATOKEO , UNAZALISHA  SABABU.
Kabla
 hata hujaanza kufanya kitu, tayari umeshatengeneza sababu za kujitetea 
utakaposhindwa kwenye kitu hicho. Hivyo badala ya kuweka nguvu zako 
kubwa kuzalisha matokeo ya ushindi unayotaka, unapeleka nguvu hizo 
kuzalisha sababu za kujitetea. Huwezi kuzalisha sababu na matokeo kwa 
pamoja, chagua kuzalisha sababu na kuachana na matokeo au kuzalisha 
matokeo na kuachana na sababu.
Kataa kuwa mtu wa sababu, kuwa mtu wa kujisukuma kwa kila namna kupata matokeo unayotaka, usiwe mtu wa kukimbilia sababu.
Sunday, March 29, 2020
Friday, March 27, 2020
Wednesday, March 25, 2020
MWONGOZO WA KUFANYIA KAZI AU KUJISOMEA KWA WANAFUNZI NYUMBANI !!
FAIDA  ZA  KUFANYIA  KAZI  / KUJISOMEA  NYUMBANI.
Kufanyia
 kazi zako nyumbani, iwe umeajiriwa au umejiajiri au  wewe  ni  
mwanafunzi wa  shule  za   msingi , sekondari  au  chuo   kuna faida 
nyingi sana, baadhi ya faida hizo ni kama ifuatavyo;
- Unaokoa muda mwingi ambao huwa unaupoteza kwa kwenda eneo la kazi, shule au chuo Kuanzia muda unaotumia kwenda, kurudi na mwingine unaopotea, kwa kufanyia kazi nyumbani hupotezi muda wako.
- Unapunguza fursa za kupoteza muda zinazopatikana kwenye eneo la kazi, mfano mikutano mbalimbali ambayo hufanyika maeneo ya kazi, ambayo kwa sehemu kubwa haina tija.
- Unafanya kazi kwa mpango wako bila ya kusumbuliwa na wafanyakazi wengine.Kama mwanafunzi au mwanachuo unaepuka kelele za wanafunzi wenzako . Japo kunakuwa na mawasiliano ya simu au njia nyingine za mtandao, ile hali ya kukatishwa na wengine wakati unafanya kazi au unajisomea inapungua.
- Kwa sehemu kubwa unakuwa na uhuru wa kupanga muda wako mwenyewe, hasa kama kazi yako haihitaji kushirikiana na wengine wakati mnaifanya. Unaweza kupanga kufanya kwa muda unaofaa kwako.
- Unapata muda mwingi wa kupumzika, majukumu yako unayofanya ukiwa kazini, shule , chuo ukiyafanyia nyumbani itakuchukua nusu ya muda unaotumia kuyafanya ukiwa kazini , shule au chuo .Hivyo unapata muda mwingi wa kupumzika au kufanya mambo mengine.
Changamoto za kufanyia kazi nyumbani.
Hakuna kisichokuwa na changamoto, na katika kufanyia kazi nyumbani, zipo changamoto nyingi. Hapa ni baadhi ya changamoto hizo;
- Kushindwa kutekeleza majukumu yako kwa wakati kwa sababu hakuna anayekusimamia moja kwa moja au anayekuangalia. Unahitaji nidhamu kali sana kuweza kujisimamia mwenyewe.
- Usumbufu wa wanafamilia wakati unafanya kazi, wengi hawajui kwamba japo upo nyumbani pia upo kazini, hivyo kuingilia kazi zako pale wanapokuwa na mahitaji mbalimbali.
- Kukosekana kwa mipaka kati ya kazi na maisha. Kwa kuwa unafanyia vyote nyumbani, ni rahisi kushindwa kuweka mipaka, ukajikuta unaruhusu mambo ya kifamilia kuingia kwenye wakati wa kazi au mambo ya kikazi kuingia kwenye wakati wa familia.
- Wageni usiokuwa na miadi nao wanapokuja nyumbani na kujua upo, wanaingilia sana muda wako wa kazi. Wengi hawawezi kuelewa kwamba japokuwa upo nyumbani, upo kazini, hivyo kuhitaji muda wako mwingi.
- Ni rahisi kwa uvivu kukunyemelea, ukipatwa na usingizi kidogo ni rahisi kwenda kulala au kufanya mambo mengine ya kupoteza muda kama kuangalia tv, kuzurura mitandaoni na kadhalika.
MKAKATI  BORA  KWAKO  WA   KUFANYIA  KAZI  NYUMBANI.
Ili
 kupata manufaa ya kufanyia kazi nyumbani, pamoja na kuzuia changamoto 
zake zisiwe kikwazo kwako, tengeneza mkakati mzuri kwako kufanyia kazi 
nyumbani
Zingatia mambo yafuatayo katika kutengeneza mkakati wako wa kufanyia kazi nyumbani utakaokupa matokeo mazuri.
( 01 ). TENGA  ENEO  LA  KUFANYIA  KAZI.
Kitu
 cha kwanza muhimu kabisa kwako kufanya ni kutenga eneo la kufanyia kazi
 ukiwa nyumbani. Huwezi kuwa unafanyia kazi kila mahali na ukawa na 
nidhamu nzuri. Badala yake unapaswa kutenga eneo ambalo utakuwa 
unafanyia kazi zako, na ukiwa eneo hilo unachofanya ni kazi tu na siyo 
kitu kingine.
Hii
 inakuandaa kisaikolojia kuheshimu eneo hilo na unapokuwa kwenye eneo 
hilo unajua cha kufanya ni kazi. Kama unaishi kwenye nyumba kubwa 
unaweza kutenga chumba utakachotumia kama ofisi. Lakini kama huwezi 
kufanya hivyo unaweza kutenga eneo kwenye chumba chochote, hata kile 
unacholala na kulitumia kama eneo la kazi.
Kama
 unatenga eneo ndani ya chumba chenye matumizi mengine, hakikisha 
unaweka kiti na meza kwa ajili ya kufanyia kazi. Hivyo unapokaa kwenye 
kiti na meza hiyo, unajua kabisa hili ni eneo la kazi. Usifanye kitu 
kingine unapokuwa kwenye kiti na meza ulivyoandaa kwa ajili ya kazi.
Epuka
 kufanyia kazi kitandani au kwenye kochi, kwenye maeneo hayo hutaipa 
kazi uzito kwa sababu kisaikolojia unayachukulia kama maeneo ya 
kupumzika
 ( 02 ). TENGENEZA  RATIBA  YAKO  YA  KILA  SIKU  NA  IFUATE.
Japokuwa
 una uhuru wa muda gani ufanye kazi unapokuwa nyumbani, uhuru huo una 
mipaka. Huwezi kufanya kazi zako pale unapojisikia, ukienda kwa mpango 
huo hutafanya chochote. Ndiyo una uhuru, lakini lazima utengeneze ratiba
 yako mwenyewe na uifuate kila siku.
Panga
 kabisa ni muda gani unaamka, ukiamka unafanya nini, muda gani 
unapumzika, unakula na unakuwa na familia. Yote hayo lazima uyapange na 
kisha kuyafuata.
Ukianza siku zako bila mpango, utajikuta umefanya mengi, umechoka lakini hakuna kikubwa ulichokamilisha.
Kwenye ratiba yako ya siku tenga kabisa masaa ambayo huhitaji usumbufu, hayo ni masaa ya kazi zinazohitaji umakini mkubwa.
( 03 ). VAA  KAMA  UNAENDA  KAZINI / SHULENI / CHUONI
Unapofanyia
 kazi nyumbani, una uhuru wa kuvaa utakavyo au hata kutokuvaa kabisa. 
Lakini hilo unapaswa kuwa nalo makini, kwa sababu lina madhara ya 
kisaikolojia kwenye utekelezaji wa majukumu yako ya kazi. Kama umevaa 
nguo za kawaida utajiona kama hauna majukumu makubwa.
Hivyo
 unapaswa kujiandaa vizuri kama vile unaenda kazini  shuleni, chuoni kwa kuvaa kabisa 
nguo zako za kazi na kisha kukaa eneo lako la kazi wakati unafanya kazi.
 Unapovaa nguo kama vile unaenda kazini, akili yako inakupa uzito wa 
kikazi na unatekeleza majukumu yako vizuri. 
( 04 ). WATU  WOTE  WAJUE  RATIBA  YAKO.
Ukishaweka
 ratiba yako ya siku, kila mtu kwenye familia anapaswa kuijua. Na 
waeleze wazi kwamba japokuwa upo nyumbani, lakini pia upo kazini au  unajisomea. Kwa 
muda ule wa kazi, mambo yote hapo nyumbani yanapaswa kuendelea kama vile
 wewe haupo kabisa.
Ule
 muda ambao umetenga usisumbuliwe, usisumbuliwe kweli, labda kwa jambo 
la dharura, ambalo hata kama ungekuwa kazini basi ungepigiwa simu. Na 
weka kabisa vigezo vya dharura ni vipi. Usipofanya hivi, watu watatumia 
uwepo wako kuuliza vitu mbalimbali na hilo kuathiri kazi zako.
Kuhusu
 wageni, kama kuna mgeni amekuja na hukuwa na miadi naye, usikutane naye
 wakati ambao unafanya kazi. Anapaswa kuelezwa ratiba yako na muda mzuri
 kwako kukutana naye. Na kama ni mgeni muhimu, unaweza kumsalimia na 
kumpa ratiba yako ilivyo na mkapanga muda gani mzuri wa kuwa na 
maongezi, kama yapo na ni muhimu.
 ( 05 ). TENGENEZA  MIPAKA YA  KAZI / KUSOMA  NA  MAISHA.
Kwa
 kuwa upo nyumbani na unafanyia kazi nyumbani, mpaka kati ya kazi na 
maisha unafutika kabisa. Wakati wa kazi utaingiliwa na mambo ya 
kifamilia na wakati wa familia utaingiliwa na mambo ya kikazi.
Ni
 lazima utengeneze mpaka kati ya kazi na maisha, ufanye kazi wakati wa 
kazi na maisha wakati wa maisha. Jisukume kutekeleza majukumu yako ya 
kazi kwa wakati uliopanga kufanya kazi na ule wakati uliopanga kupumzika
 au kuwa na familia basi usiruhusu kazi au  masomo kuingilia wakati huo.
( 06 ). TUMIA  VIFAA  VYA  KUONDOA  USUMBUFU.
Kama
 mazingira ya nyumbani kwako siyo rafiki kwako kupata utulivu wa kazi au kusoma, 
labda kuna kelele mbalimbali za majirani na watu wengine, basi tumia 
vifaa vya kuondoa usumbufu.
Hapa
 unapaswa kuwa na spika za masikioni (headphone au earphone) ambazo 
utazivaa wakati wa kufanya kazi. Kuna ambazo zina sifa ya kufunga kelele
 za nje zisikuingie na hivyo kukupa utulivu mkubwa wa kufanya kazi zako.
Pia
 kitendo cha kuvaa spika hizo, kinamfanya mtu asikusemeshe mara kwa 
mara, kwa sababu anajua humsikii. Pia mtu anapokusemesha, jifanye kama 
humsikii, hata kama unamsikia, hasa pale jambo linapokuwa siyo muhimu.
Inayoendana
 na hii ni kuandaa orodha ya nyimbo (playlist) zinazokupa utulivu na 
kuitumia wakati unafanya kazi zako. Hapa unasikiliza nyimbo hizo kwa 
kujirudia rudia na hilo linafanya akili yako izame kwenye kazi 
unayofanya na kuepuka usumbufu.
 ( 07 ). JALI  AFYA  YAKO.
Unapofanyia
 kazi nyumbani, kama kazi zako ni za kutumia akili na unazipenda sana, 
unaweza kujikuta umekaa kwenye kazi siku nzima na hujatoka kabisa nje ya
 nyumba yako. Pia ulaji ni rahisi sana unapokuwa nyumbani kuliko ukiwa 
kazini, ni rahisi kula mara kwa mara ukiwa nyumbani kuliko ukiwa kazini.
Hivyo
 unapaswa kuwa na mkakati wa kujali na kuboresha afya yako. Kitu cha 
kwanza muhimu ni kufanya mazoezi, tenga muda wa kufanya mazoezi ambayo 
yatakutoa jasho. Cha pili ni kudhibiti ulaji, usile kwa sababu kuna kitu
 cha kula, bali kula kwa utaratibu maalumu na kuwa makini na kile 
unachokula. Cha tatu ni muda wa kupumzika, unaweza ukakosa mapumziko 
mazuri japo uko nyumbani na hilo likaathiri afya yako.
 (08 ). PANGILIA  MUDA  UNAOENDANA  NA  WEWE  NA  UNAOEPUKA  USUMBUFU.
Kitu
 kimoja ambacho kimekuwa kinanisaidia sana mimi binafsi kuweza 
kukamilisha sehemu kubwa ya uandishi ni kutenga muda wa uandishi ambao 
unaendana na mimi na pia unaepuka usumbufu.
Huwa
 ninaamka saa kumi kamili asubuhi kila siku na baada ya kufanya tahajudi
 na tafakari kisha kuipangilia siku, kuanzia saa kumi na nusu mpaka saa 
12 kamili huo ni muda wa kuandika tu, sifanyi kingine kwenye muda huo. 
Kwa muda huo, nimekuwa na uwezo wa kuandika kwa kiwango kikubwa sana, 
kwa sababu akili inakuwa na utulivu na hakuna usumbufu, maana watu 
wengine wanakuwa wamelala kwenye muda huo.
Hivyo
 na wewe pangilia majukumu yanayohitaji utulivu na umakini kulingana na 
wewe binafsi na mazingira. Yaani yapange kwenye muda ambao akili yako 
iko vizuri lakini pia hakuna usumbufu wa nje.
Watu
 tumegawanyika kwenye makundi mawili; kuna ambao wanaweza kuamka asubuhi
 na mapema na akili zao zikawa vizuri (early birds) na kuna ambao 
wanachelewa kulala na muda wa usiku ndiyo akili zao zinakuwa vizuri 
(night owls). Jijue wewe uko kundi gani, kisha tenga muda ambao wengine 
wamelala na ufanye kuwa wa kazi.
Mfano
 kama uko vizuri kwenye kuamka asubuhi basi amka asubuhi na mapema sana,
 labda saa tisa au saa kumi na kisha tumia masaa mawili ya kwanza kwenye
 kazi inayohitaji umakini wako na utulivu. Muda huo wengi wanakuwa 
wamelala na hivyo usumbufu unakuwa mdogo.
Na kama unachoelewa kulala basi tenga masaa mawili ya usiku mnene ambapo wengine wamelala na akili yako imetulia kufanya kazi.
Ukiweza
 kutenga masaa mawili ambapo akili yako imetulia na ina umakini na 
hakuna usumbufu wa nje, kisha kuyaweka masaa hayo mawili kwenye kazi, 
utatekeleza majukumu makubwa kuliko anayefanya kazi siku nzima kwenye 
ofisi isiyo na utulivu.
Rafiki
 yangu mpendwa, mdau  wangu  huu ndiyo mwongozo sahihi kwako wa kufanyia kazi 
nyumbani .(  kama  wewe  ni  MWAJIRIWA , UMEJIAJIRI , MWANAFUNZI , MWANACHUO  ni  mwongozo  mzuri  sana  kuufuata.
MBINU NA KANUNI ZA KUSOMA NA KUFAULU MITIHANI
UTANGULIZI
Kila mzazi angependelea mwanae afanikiwe katika masomo na kufaulu mitihani yake. Pia kila mwanafunzi anahitaji kufaulu katika mitihani yake. Walimu nao hujisikia vizuri wakati wanafunzi wao wanapofanya vizuri katika mitihani yao.
Kufaulu mtihani ni muhimu kwa malengo ya mwanafunzi, kwani
anaposhinda mitihani humwezesha kuwa na mtazamo wa juu kielimu, kwa mfano kupata
cheti, diploma au digrii, kitu ambacho humfanya afae kwenye kazi. Wakati
mwingine inakuwa ni viguinu kwa baadhi ya wanafunzi kumudu masomo na mitihani
yao. Wakati huohuo wapo baadhi yao ambao wao kufaulu mitihani si tatizo.
 
Sasa mtu anaweza kujiuliza, kwa nini wanafunzi wengine washindwe
na wengine wafaulu vizuri katika masomo na mitihani yao? Mafanikio katika masomo
na kufaulu mitihani kunahitaji uwezo wa asili, kufanya kazi kwa bidii na kufuata
kanuni na mbinu za kusoma.
Wanafunzi wengine huona ugumu katika masomo na kufaulu mitihani,
si kwa sababu hawana akili, bali hawafuati mbinu na kanuni ftilani za kusoma na
kufaulu mitihani. Wengi wana uwezo mzuri, kama watajifunza mbinu hizi. Mbinu na
kanuni hizi zinaweza kutumiwa na wanafiinzi wa shule za msingi, sekondari, vyuo
na hata vyuo vikuu.
 
Kanuni na   mbinu  za Kusoma ni kama ifuatavyo: 
 JIJENGEE   NIDHAMU BINAFSI  YA  HALI  YA  JUU  YA  KUJISOMEA   KILA  SIKU.
 -----Weka lengo maalum
la kusoma kila siku na litimize.
 -----Weka ratiba ya kila somo na
ifuate. 
-----Tenga muda wa kutosha kwa kila
somo.
----- Jiwekee muda wa kutosha kila
siku kwa ajili ya kazi za utoaji taarifa za masomo na projekti. 
 -----Uwe na mahali maalumu pa
kusomea.   
------Epuka kitu chochote
kinachoweza kukufanya usisome vizuri.
 ---- Jisomee katika muda unaodhani
unataa zaidi.
 -----Uwe na muda wa kupumzika kila
unapochoka kusoma.
----- Usifanye mambo mengi kwa
wakati mmoja. Kwa mfano, mapenzi au anasa za kimwili wakati ungali mwanafunzi.
Hivyo ni vikwazo masomoni.
---- Tafuta mahali pasipo na kelele
za aina yoyote.
----- Epuka vishawishi vinavyoweza
kukufanya uairishe kujisomea. 
------Fanya mazoezi ya mwili mara
kwa mara.
 JIANDAE  MUDA  WOTE SOMA  KILA   WAKATI  NI   MUDA   WA   KUSOMA---USIPOTEZE   MUDA. 
-----Kabla hujaanza kujisomea,
hakikisha kuwa zana zote muhimu kwa kusomea zipo.
----- Hakikisha kuwa mahaii pa
kusomea pana mwanga wa kutosha.
----- Epuka kusoma ukiwa umejilaza
kitandani.
----- Unapokuwa na matatizo
kimasomo, mwone mwalimu, anayehusika.
------ Uwe na muda mwingi wa
kujisomea kila siku, usipoteze muda kwa mambo yasiyo ya lazima kama vile
maongezi.
------ Jiandae kwa mtihani kila
wakati, usingoje mwalimu atangaze kuwa ataleta mtihani ndipo usome.
----- Epuka kusoma hadi usiku sana;
utaharibu afya yako. 
------ Hudhuria shughuli zote za
shule nje ya darasani. 
KUWA   KING" ANG"ANIZI , PIGANA , KOMAA , PAMBANA, KUWA   MBISHI---USIKATE   TAMAA   
----Jenga tabia ya uvumilivu na
kamwe usikate tamaa wakati ugumu unapoibuka masomoni.
---- Jenga tabia ya kupania kufaulu
katika masomo yako.
----- Amini kuwa utafaulu.
-----Epuka kuwaonea wivu na
kujilinganisha na wengine kimasomo, bali, jifunze tu siri za mafanikio yao.
-----Chunguza masomo yao ili ujue
udhaifti wako uko wapi.
 
     WAKATI  UNAPOKUWA  SHULENI  , CHUONI   
----Fika darasani kwa wakati
unaotakiwa ili usikose maagizo.
----Usikose kipindi bila sababu
maalumu. 
 ---Wakati mwalimu hajafika
darasani, pitia yale uliyojifunza kipindi kilichopita.
----Usisome mambo mengi kwa wakati
mmoja.
 ---Soma kazi zako zote za
darasani kabla ya kuanza darasa.
 ---Usiwe mtu wa kukaa tu
darasani, uliza na jibu maswali yanapoulizwa. 
 ---Uwe mwanafunzi mdadisi wa
mambo kwa walimu na hata kwa wanafunzi wenzako pia. 
----Wasilisha kazi za darasani kwa
wakati wake.
----Baada ya kipindi, pitia yale
uliyojifunza.
----Epuka kukaa kimya na nyuma ya
darasa, bali shiriki katika mazungumzo ya darasani na wenzako.
---- Jenga uhusiano mzuri kwa
walimu wako na kwa wanafunzi wenzako. Ukiwa na amani moyoni, utasoma na kuelewa.
Jistahi na kuwapenda walimu wako. Ukimpenda mwalimu utalielewa vizuri somo lake.
JINSI  YA  KUJIFUNZA  LUGHA  YOYOTE  YA   KIGENI--Mfano :-Kiingereza , Kifaransa , Kichina , Kijerumani , n.k  
-------Kama unajifunza lugha ya
kigeni, Fanya marudio, mazoezi mengi na soma vitabu vingi vya hadithi vya lugha
hiyo.-
------ Soma ukiwa na kamusi na tafuta
maana ya neno usilolijua.
----- Jizoeze kusikiliza na kuongea
ukiwaiga wajuao ujifunzapo lugha ya kigeni.
-----Sikiliza mihadhara na redio
ili ujifunze kwa wengine wanavyotamka maneno.
-----  Jikumbushe maneno magumu kila
siku.
------ Kila nafasi unayoipata itumie
kwa kusoma.
------ Pambana na sarufi za lughaya
kigeni kikamilifu.
------ Jifunze lugha ya kigeni kwa
kuongea mara kwa mara.
------- Ni jambo la busara kuwa na
usiku mmoja wa kupunzika katikajuma ambayo si Jumapili au Jumamosi. 
JIHUSISHE    NA  WENGINE  UNAPOKUWA    MWANAFUNZI(  JIJENGEE  TABIA  NJEMA ) 
----- Ni muhimu kujihusisha na watu
wengine, jambo hili litakufariji kimawazo.
-----Ni vizuri pia kuwa na
mwanafunzi mwenzio wa kujadili naye.
EPUKA    HAYA  UKIWA   MWANAFUNZI    
-----Epuka marafiki wabaya wenye
nia ya kukupotosha.
-----Epuka pombe, uvutaji wa
sigara, bangi na madawa ya kulevya. Huharibu ubongo na kudhoofisha afya.
----Jijengee tabia njema ya
kujizuia katika tamaa za mwili.
 ------Kabla ya mtihani, soma kwa
bidii sana usingoje mtihani umekaribia ndipo usome.
 
--------Usiku unaofuatiwa na siku ya
mtihani uwe na muda wa kutosha wa kulala. Usisome hadi usiku wa manane.
------  Soma kwa mpangilio kila siku
ili kujiandaa kikamilifu kwa mtihani.
--------Siku ya mtihani, usifikirie
kushindwa bali uwe na imani kuwa utashinda. Ondoa wasiwasi na mashaka.
------  Wahi kwenye chumba cha mtihani
kwani kuchelewa huleta hofu.
------ Chukua vifaa vyote muhimu
katika mtihani kama vile kalamu, penseli na rula. 
 ----- Soma maagizo ya mtihani kwa
uangalifu sana, na hakikisha uko makini kwa kile unachotakiwa kufanya kabla ya
kujibu swali lolote. 
-----Kabla hujaanza kujibu maswali,
angalia maswali ambayo ni rahisi kwako kujibu..
-----Jibu maswali rahisi kwanza na
kwa haraka ili upate muda wa kutosha kujibu maswali
magumu.
 ----------------------------------------------------------------------------------
           "USHINDI    NI    WAKO   UNASTAHILI "
TUPO PAMOJA, TUTAKUTANA KILELENI. SEE YOU AT THE TOP
Ndimi 
Rafiki na  Kocha  Wako  Mwl    Japhet 
Masatu , Dar  es  salaam ,Tanzania , Afrika   Mashariki
, 
Mwl   Japhet   Masatu  ni  
Mwalimu  Kitaaluma , Kocha  wa Maisha  na   Mafanikio
,  Mshauri , Mwalimu,  Mjasiriamali , Public 
Speaker
 KWA  MAELEKEZO    ZAIDI  TUWASILIANE   KWA
WhatsApp / Call / Message + 255 716 924136 / + 255 755 400128 / + 255 688361539
Tuma   MAONI , USHAURI , CHANGAMOTO  KWA  EMAIL :
studentsgotz.9@gmail.com 
Sunday, March 22, 2020
Saturday, March 21, 2020
Friday, March 20, 2020
Thursday, March 19, 2020
Wednesday, March 18, 2020
Tuesday, March 17, 2020
Monday, March 16, 2020
Sunday, March 15, 2020
Wednesday, March 11, 2020
Monday, March 9, 2020
Sunday, March 1, 2020
Saturday, February 22, 2020
Saturday, February 15, 2020
Sunday, February 9, 2020
Friday, February 7, 2020
Wednesday, February 5, 2020
Saturday, February 1, 2020
Friday, January 31, 2020
Tuesday, January 28, 2020
Sunday, January 19, 2020
Wednesday, January 15, 2020
Tuesday, January 14, 2020
Monday, January 13, 2020
Saturday, January 11, 2020
Saturday, January 4, 2020
Thursday, January 2, 2020
Wednesday, January 1, 2020
Sunday, December 29, 2019
Saturday, December 28, 2019
Thursday, December 26, 2019
Wednesday, December 25, 2019
Tuesday, December 24, 2019
Sunday, December 22, 2019
Wednesday, December 18, 2019
Tuesday, December 17, 2019
Monday, December 16, 2019
Subscribe to:
Comments (Atom)
 
