Friday, October 3, 2014

JOKA LA MDIMU A.J. Safari{ H.P}---KIDATO CHA 3 NA 4

                                         UHAKIKI---RIWAYA

                                      JOKA    LA    MDIMU
MWANDISHI:  ABDALA  .J.   SAFARI{H.P.}
MCHAPISHAJI: HUDA  PUBLISHERS.
MWKA: 2007.


UTANGULIZI
RIWAYA    YA   JOKA  LA   MDIMU  ni   riwaya  ambayo   inaakisi  vizuri   matatizo    ya   KIUCHUMI  ya  miaka   ya   themanini  nchini  TANZANIA.  RIWAYA   hii  inaakisi   tu ,  haihakiki ,  hali  ya   maisha  katika  kipindi  cha  dhiki   ya ukosefu  wa   bidhaa   muhimu  kama   vile   nguo,  chakula ,  mafuta ,  spea  za   mashine  n.k. Wakati  huu  wa   dhiki  watu   wengine   wanateseka    na   kuumia ,  kuna   wengine    wachache   wanaotumia   nafasi   zao   kuchuma  kadri   wanavyoweza ,  hasa  kwa  njia  haramu.



UHAKIKI   WA   MAUDHUI


DHAMIRA   KUU:  Hali  ngumu   ya   Maisha.

DHAMIRA   NYINGINEZO
{1}.Rushwa   katika   jamii.
{2}.Urasimu.
{3}.Kutowajibika.
{4}.Nafasi  ya  Mwanamke katika  jamii.
{5}.Mapenzi   na Ndoa.
{6}. Uhujumu  Uchumi  na   Magendo.
{7}. Ufisadi.

WAHUSIKA

{1}. AMANI---Huyu  ni   mhusika  mkuu. Ni  dereva   taksi.  Ni  kijana  mchapa  kazi.  Ana   huruma. Ana  hekima  na   busara.Anafaa  kuigwa  na   jamii.

{2}. GRAY  KWACHA---Huyu  ni   mhusika  msaidizi. Ni  mkurugenzi   wa   Idara   ya   Fedha   za   Kigeni. Ni   malaya. Si  mtu  adilifu.  Ni  fisadi.  Anapenda  rushwa.Anafanya   biashara  za   magendo. Hafai   kuigwa.

{3}. TINO---Huyu  ni   mhusika  mkuu   msaidizi.  Ni   mvuta  kwama. Ni  baba   wa   watoto  watatu.  Ni  jasiri. Ni  mchapa   kazi.  Mwanamichezo.  Anafaa  kuigwa.

WAHUSIKA   WENGINE:

----JINJA   MALONI , DAKTARI  MIKWALA ,SHIRAZ   BHANJ ,  ZITTO ,CHECHE ,

No comments:

Post a Comment