Monday, March 10, 2014

KISWAHILI KIDATO CHA KWANZA --- BY. MWL. JAPHET MASATU.

FASIHI  SIMULIZI.


FASIHI SIMULIZI
Utanzu wa Fasihi
Kiingereza Oral Literature
Tanzu za Fasihi Simulizi

Prev Tamathali za Usemi
Next Fasihi Andishi
VIPERA VYA TANZU ZA FASIHI SIMULIZI
HADITHI / NGANO
NYIMBO
  • Mashairi
  • Kimai
  • Wawe/Hodiya
  • Nyimbo za Ndoa
  • Nyimbo za Kidini
  • Nyimbo za Kisiasa
  • Za Tohara/Jandoni
  • Nyimbo za Kizalendo
TUNGO FUPI
MAIGIZO
Fasihi Simulizi ni utanzu wa fasihi ambao unawakilisha sanaa ya lugha inayopitishwa kutoka kwa kizazi hadi kizazi kwa njia ya maneno/masimulizi ya mdomo.

Sifa za Fasihi Simulizi

  1. Hupitishwa kwa njia ya mdomo
  2. Ufanisi wa sanaa katika fasihi simulizi hutegemea uwezo wa msimulizi, au wahusika
  3. Masimulizi yake yanaweza kuathiriwa na mazingira, hisia na hali
  4. Ni mali ya jamii. Hakuna mtu fulani anayemiliki sanaa katika fasihi simulizi.
  5. Inaweza kubadilika kutoka kizazi hadi kizazi, au mazingira mbalimbali kwa sababu hutegemea kumbukumbu ya msimulizi.
  6. Aghalabu huwa na funzo fulani

Umuhimu wa Fasihi Simulizi

  1. Kuburudisha - Hufurahisha na kuchangamsha hadhira
  2. Kunasihi- kutolea mawaidha na kuonyesha mwelekeo unaotarajiwa katika jamii
  3. Kuelimisha watu kuhusu vitu mbalimbali hasa mazingira yao
  4. Kutambulisha jamii - jamii mbalimbali husifika kutokana na sanaa zao katika fasihi simulizi kama vile nyimbo
  5. Kuhifadhi na kudumisha utamaduni wa jamii
  6. Kuunganisha watu - huleta watu pamoja
  7. Kukuza lugha - fasihi huimarisha lugha kwa kuwa hutumia mbinu mbalimbali za lugha.
  8. Kuliwaza - hutoa huzuni na kuleta matumaini.
  9. Kupitisha muda - wakati mwingine fasihi simulizi hutumika kupitisha muda.

FASIHI  KWA  UJUMLA.

FASIHI
Katika uga wa fasihi kuna kumbo tatu muhimu zinazoipa uhai taaluma nzima ya fasihi. Kumbo hizo ni ushairi, riwaya na tamthiliya. Uwe ukweli ama kinyume chake lakini jambo la muhimu kufahamu ni kuwa kila kumbo katika fasihiutawaliwa na kanuni zake na nijambo la kiuungwana kuzifuata kanuni au Jadi husika. Kanuni hizo hutoa muongozo katika utungaji wa kazi za kifasihi na uhakiki wa kazi hizo. Aghalabu kuzitumia kanuni huwa ni jambo la Kiuugwana na la kheri, lakini katika zama tulizonazo sasa sio dhambi kubwa ya kiuandishi ahesabiwayo mwandishi na wanamapokeo anapokiuka jadi husika katika kumbo mojawapo ya fasihi andishi.
Tunapozungumzia kanuni ama Jadi ya kiutunzi katika uga wa fasihi tunamaana ya mambo yajitokezayo na kurudiwarudiwa mara kwa mara katika kumbo fulani ya fasihi, kwa mfano, mambo yajitokezayo mara kwa mara katika kumbo ya tamthiliya ni utumizi wa jukwaa, hadhira, wahusika, mtiririko wa vitendo, dhamira na nyimbo. Kama wasemavyo waswahili “Kawaida ni kama Sheria”, ndivyo hivyo mambo hayayanayojirudia katika kila kazi ya kitamthiliya ndiyo yajengayo kanuni ama sheria za utungaji wa tamthiliya.
Hapo mwanzo kabla ya kuibuka kwa fasihi ya Kiswahili ya majaribio, kanuni zote za ujenzi wa tamthiliya ya Kiswahili zilikopwa kutoka katika tamthiliya ya Ulaya. Vyanzo vingi vya taarifa vinaeleza kuwa kanuni hizi za ujenzi wa tamthiliya ziliwekwa na wanataaluma wa kimagharibi lakini ukweli ni kwamba chimbuko la tamthiliya katika nchi na tamaduni mbalimbali hushabihiana kwa kiasi kikubwa kwa vile uhusishwa na visakale na matendo ya kidini. Kwa mfano, yasemekana kuwa huko Ulaya tamthiliya ilitokana na miviga na viviga, hasa ya kidini, katika jamii ya kale ya Wayunani, (Holman 1972, katika Mulokozi1996). Miviga hiyo iliambatana na duru za kuzaliwa, kukua, kufa, kuoza na kuzaliwa upya ambazo hasa zilihusishwa na Mungu aliyeitwa Dionizi, aliyeaminiwa kuwa aliuawa, akakatwakatwa vipandevipande na baadaye akafufuka tena (Mulokozi 1996). Pia hapa Afrika, kumbukumbu za kwanza za maigizo ya kitamthiliya tunazipata Misri, ambako michezo ya miviga ilihusu kufa na kufufuka kwa Mungu wa Wamisri aliyeitwa Osiris ilikuwa ikiigizwa kila mwaka kwa miaka 2000 kuanzia kama mwaka 2500KM, (Mulokozi 1996). Hii inaonyesha kuwa chimbuko la tamthiliya katika jamii nyingi duniani linashabihiana kwa kiasi kikubwa. 
Kanuni zilizowekwa juu ya ujenzi wa tamthiliya zilitokana na mambo yaliyopelekeachimbuko la tamthiliya. Inaonekana wazi kuwa kanuni hizi zilihusika na zinaendelea kuhusika kwa kiasi kikubwa katika kujenga muktadha, fani na vitendo vitendekavyo katika matambiko na mikusanyiko ya kidini, kanuni hizo kama vile utumizi wa jukwaa, hadhira, wahusika, vitendo, dhamira na nyimbo zinahusika moja kwa moja katika matendo yatendekayo katika matambiko, miviga na dini za kijadi na zile za kigeni.
Kanuni huwa hazibakii hivyohivyo, hubadilika kufuatana na mahitaji ya jamii kwa wakati fulani. Hapo mwanzo kanuni za Ki-Aristotle zilitumika vizuri na kwa usahihi katika utanzu wa tamthiliya ya kiswahili. Kadri siku zilivyoenda mbele watunzi wa tamthiliya ya Kiswahili walilazimika kukiuka baadhi ya kanuni hizo kwa kuingiza vipengele vya fasihi simulizi katika tamthiliya ya kiswahili ili kuifanya tasnia ya tamthiliya andishi ifungamane na uhalisi wa kiafrika. Waandishi wengi wa tamthiliya tulionao sasa ni wafuasi wazuri wa kukiuka kaida za Ki-Aristotle, ndipo sasa tunaona umuhimu mkubwa wa utafii huu. Vile vile ikumbukwe kuwa uandishi huu wa “Kimajiribio”au ukiukwaji huu wa kaida za kiuandishi umejitokeza katika kumbo zote za fasihi andishi, lakini utafiti huu umeshughulikia kumbo ya tamthiliyatu.
Ukiukwaji wa kaida za Ki-Aristotle na kuingizwa kwa kanuni za U-jadi (wataalamu wengine wanazitambulisha kanuni za U-Jadi kama fasihi ya kiswahili ya majaribio), katika uandishi wa tamthiliyaya Kiswahili umeibua maswali mengi kwa wadau wa fasihi.
F.E.M.KSenkoro(2011:62) anajadili baadhi ya maswali hayo, hapa anasema “Swali ambalo hatimaye linajadiliwa ni; je, majaribio haya yanafuata kanuni zipi? Upya una nafasi gani katika majaribio? Na, Je, majaribio mahsusi ya fasihi fulani yanaanza na kuisha wakati gani?
Senkorohajatoa ufafanuzi wakutosha juu ya maswali haya. Mambo mengi ameyaacha hewani. Utafiti huu umeibuka na majibu kwa baadhi ya maswali na kuyaacha mambo mengine kama mada za utafiti kwa watafiti tarajali.
Kuna tafiti kadhaa zilizofanywa na kuhifadhiwa zinazohusu tamthiliya ya Kiswahili, tafiti nyingi kati ya hizi zinahusu uchambuzi wa vipengele vya fani na maudhui ndani ya tamthiliya teule. Hata hivyo kwa upeo wa ufahamu wa mtafiti hakuna mtafiti aliyewahi kujishughulisha kuhusu mabadiliko ya uandishi wa tamthiliya ya Kiswahili kutoka U-Aristotle kwenda U-Jadi wa Kiafrika. Wapo watafiti ambao wamefanya utafiti kuhusu tamthiliya kwa kuchambua vipengele mahususi,baadhi ya watafiti hao ni Omary (2011), alichunguza suala la Ukimwi lilivyo jadiliwa katika tamthiliya za Kiswahili, Murusuri (2011), alitazama Utamthiliya katika Ngonjera, data mahsusi alizitoka ndani ya vitabu vya Ngojera za Ukuta, Ngojera hizi zimetungwa na mwasisi wa chama cha UKUTA na mshairi mashuhuri Mathius Mnyampala. Vielevile, Madembwe (2011), alifanya utafiti juu ya nafasi ya kejeli na dhihaka katika tamthiliya za Penina Muhando. Kwa upeo wa ufahamu wa mtafiti wa utafiti huu ni kwamba hakuna mtafiti aliyewahi kuchunguza juu ya mabadiliko ya kiuandishi yaliyojitokeza katika tamthiliya ya Kiswahili kutoka uandishi unaofuata kanuni za Ki-Aristotle kwenda katika uandishi wenye kuzingatia vipengele vya Jadi ya Ki-Afrika. Kwa upeo wa mtafiti wa utafiti huu, mtafiti mmoja tu ndiye aliyejaribu kujadili baadhi ya matendo ya kiafrika ndani ya tamthiliya ya Kiswahili. Mtafiti Nicholaus, A, alichunguza jinsi falsafa ya Ubuntu inavyo jadiliwa katika tamthiliya ya Kiswahili.
Nicholaus (2011), aliteuwa tamthiliya za Penina Muhando na kuchunguza jinsi falsafa ya Ubuntu ilivyosawiri katika tamthiliya hizo. Malengo yake ya kufanya utafiti yalikuwa ni pamoja na kuelezea mbinu alizozitumia mwandishi Penina Muhando katika kueleza masuala ya waafrika ikiwemo na falsafa yao.
Katika kutekeleza lengo hilo mtafiti alitumia tamthiliya tatu za Mama Muhando, tamthiliya hizo ni Hatia, Heshima Yangu naTambueni Haki Zetu. Matokeo ya utafiti huu yanaonyesha kuwa falsafa ya Ubuntu imejitokea kwa kiasi kikubwa katika tamthiliya za Penina Muhando. Masuala ya waafrika yamewasilishwa kwa njia mbalimbali kama vile Ngoma, kicheko, kilio, kiapo, mizimu na kwa kupitia njia ya uundaji wa chama cha ZETU, kwa kutumia njia hizi mtafiti anayataja mambo ya waafrika yaliyojitokeza zaidi ndani ya tamthiliya teule kuwa ni pamoja na ndoa za kiafrika, burudani, hekima, upendo, heshima, ushirikiano na kadhalika.
Pamoja na mtafiti kufanikiwa kuonesha mambo kadhaa yanayowahusu waafrika ndani yatamthiliya teule lakini hakuweza kuyaelezea mabadiliko ya kiuandishi katika tamthiliya ya Kiswahili. Hakutuonesha sababu zilizopeleke waandishi wengi wa tamthiliya ya Kiswahili kukiuka kaida za uandishi wa Ki-Aristotle na kuzama katika Ujadi wa Ki-Afrika, hivyo kulikuwa na haja ya kufanya  utafiti kama huu unaohusu mabadiliko ya uandishi wa tamthiliya ya Kiswahili ili kupata data na taarifa sahihi na za kutosha ili zitumike katika uwanja wa fasihi andishi.
Mbali na hayo, Nicholaus alifanya Utafiti wake kwa kuchambua kazi za mwandishi mmoja wa tamthiliya ambaye ni Penina Muhando. Utafiti huu uliona ni vema kuchambua kazi za waandishi wawili ambao kwa hakika wanamchango mkubwa katika kustawi kwa tasnia ya tamthiliya andishi ya Kiswahili. Utafiti huu umechambua kazi za Ebrahim Hussein na Penina Muhando jambo lililomwezesha mtafiti kuongeza mawanda ya kiuchambuzi na ukusanyaji wa data katika kukamilisha utafiti huu. Pia uteuzi wa vitabu vilivyo chambuliwa na kupelekea upatikanaji wa data za msingi, ni tofauti na uteuzi uliofanywa na watafiti wengine kwakuwa utafiti huu umezingatia vipindi viwili muhimu katika uandishi wa tamthiliya, kipindi cha utawala wa kanuni za Ki-Aristotle na kipindi cha pili ni hiki tulichonacho sasa (kipindi cha fasihi ya Kiswahili ya kimajaribio).

No comments:

Post a Comment