MAKALA   hii   nimeiandika 
maalumu  kwa  watanzania na 
wadau  wangu   wote ,
wanafunzi wa SHULE  ZA  MSINGI , SEKONDARI,  na   VYUO  wanaopenda  
 kujifunza  LUGHA 
YA  KIINGEREZA  na lugha 
nyingne  ngeni   KUJIFUNZA   MBINU NA  KANUNI   za   kuikuza  LUGHA   hii lengo  ni  KUWEZA   KUANDIKA 
na  KUONGEA  kwa 
UFASAHA  na  UMAHIRI   LUGHA  YA  KIINGEREZA.  
       Limekuwa  ni 
tatizo  kubwa kwa  Watanzania wengi na  wanafunzi wetu kuanzia  ELIMU AWALI, MSINGI,SEKONDARI , VYUO  kutoweza 
  kuongea  KIINGEREZA 
kwa  ufasaha   na 
umahiri.Hata   Lugha  ya 
KISWAHILI  ingawa   ni 
lugha   yetu  ya 
taifa   bado  ni 
tatizo  kwa  watanzania 
wengi  na  wanafunzi 
 kuongea   kwa 
ufasaha na  umahiri !  TATIZO 
NI  NINI ? UTAKUZAJE  UWEZO  
WAKO  WA  LUGHA ? Kujifunza  LUGHA  yoyote  
ni   suala  
ENDELEVU {long and permanent  term
}  na 
siyo   suala  la 
KUJIFUNZA  LUGHA  KWA 
WIKI  TATU  TU, 
AU    MIEZI  MITATU 
TU  ,AU   MIEZI  
SITA  TU ! KAMA  MATANGAZO 
YA  BIASHARA   YANAVYOJITANGAZA . “ JIFUNZE  LUGHA  
YA  KIINGEREZA   KWA 
WIKI  TATU “ hii   si  
kweli    ndugu   yangu.
          LUGHA  ni 
mtaji , inaweza  
kukufanikisha  mambo   yako  
katika  maisha !  Ndugu 
yangu  MTANZANIA  kama  
wewe  ni  mbumbumbu 
wa  Lugha   ya  
KISWAHILI  au   KIINGEREZA 
utachina   au  utakwama  
katika   masuala    yako  
yanayohitaji  UMAHIRI  katika  
lugha   hizo   mbili . Kuna   umuhimu  
sana   kwa   ndugu  
yangu  MTANZANIA  kuwa 
MAHIRI  katika  kutumia  
KISWAHILI  au  KIINGEREZA 
kwa  ufasaha na  umahiri .
      SIRI 
  ZA   KUIKUZA   
LUGHA  YA  KIINGEREZA
---Huwezi  kuimiliki 
lugha  yoyote  kama 
huitumii.Mtu  anaweza  kujidai 
kuwa  kwa   vile 
ni   mswahili   na  
amezaliwa  katika   lugha  
hii  basi   anaijua 
lugha. Hii  si  kweli  
kabisa   ndugu  yangu .Kama  
ingekuwa  hivyo  basi  
wote   tungeweza  kutumia 
na  kuielewa   MISAMIATI 
na   MISEMO  yote  
ambayo  iko  katika 
lugha  yako.Kwanini  basi  
wengine   wakiitumia   MISEMO  
na   MISAMIATI  hito   
wewe  unatoka   kappa , ni 
kwa  sababu  huitumii.Kwa 
hiyo   jambo  la  
msingi  ni  kuhakikisha  
kuwa   unaitumia  lugha.
----Kwa 
wale   wanaojifunza  lugha 
ya  kigeni ,  jambo 
la  msingi  ni  kuhakikisha 
kuwa  unaitumia  ili 
uweze  kupata  uzoefu  
na  hatimaye  kuitumia 
kadri   unavyotaka.
-----KUITUMIA  LUGHA 
MAANA   YAKE   NINI ? 
Izungumze  au  itumie 
katika  MAANDISHI ; kama   ni 
lugha   ngeni  kwako.Kadri  
unavyoendelea  kuitumia  katika 
mazungumzo  au   katika 
kuiandika  basi   unakuwa 
na  uwezo  wa  
kuielewa  na   utahitajika  
kupata   misamiati  mipya.
----Hudhuria  katika 
mikutano  na  uhakikishe  
unatafuta   nafasi  ya  
kuzungumza. Unapozungumza 
katika   matukio   kama 
hayo   maana  yake  
utapaswa   kuchagua   MANENO/ MISAMIATI  na  
kuyapanga  ili  uonekane  
unajieleza  kwa  ufasaha  
na   kile   kinachokusudiwa. UWEZO  WA  
LUGHA  UTAHITAJIKA.
-----Makongamano , au  hata 
ubishi   wa  kawaida  
mitaani  ni  nafasi 
nzuri  kwako   wewe  
kuitumia  ili   uweze  
kukuza  uwezo  wako 
wa  lugha. Na   wewe  
uingie  katika  ubishi 
halafu   uangalie , fanya  tathmini , baadaye , kwa   nini  
ulishindwa   au  kushinda, kwa   nguvu 
ya   hoja   au 
kwa   hoja  ya  
nguvu.Kama  unamiliki   lugha 
unaweza    KUSHINDA   kila 
KONGAMANO.
-----Jifunze  kutunga  
HADITHI  au  kuzisoma , 
KUTUNGA  MASHAIRI.Haya  ni 
mambo   pekee   yanayoweza 
kukufanya   uhitaji   uwezo 
mkubwa  wa   lugha 
na  hazina  kubwa  
ya   MISAMIATI.
 UTATUNGAJE   MASHAIRI   
KAMA   MISAMIATI   YAKO  
NI  MICHACHE ?
Aidha  ukitunga   MASHAIRI 
au  HADITHI   utajikuta  
nyakati  zote   unatafuta  
KAMUSI  au   VITABU  
vya   MISEMO   na 
lugha   ili   uweze 
kupata  MANENO   yanayofaa 
katika   utunzi  wako 
kwa  ajili  hii  
LUGHA  yako  inakua  
kwa  haraka  sana.
     Lakini  zuri  
sana   hapa   ni 
kuwa  kadri    unavyoendelea   kujihusisha 
na  utunzi  wa  
MASHAIRI  au  HADITHI   UNATUMIA 
MUDA   MWINGI  KUFIKIRI , 
na  jinsi   unavyoendelea   kushughulika   na 
mambo  hayo, uwezo  wako 
wa   KUFIKIRI  NA KUTAFAKARI 
nao  huongezeka.  Ongezeko  
la  uwezo wako   wa  
KUFIKIRI  ni   matokeo  
ya  kuwa   na  
UWEZO   MKUBWA   WA 
LUGHA.
----SIKILIZA , Wengine   hudhani  
KUSIKILIZA  sio  sehemu  
ya  kutumia /  kujifunza LUGHA.
-----FUNGULIA   REDIO, utasikiliza  MISEMO  
na  MISAMIATI  mbalimbali   
ambayo     utahitajika  kuielewa 
ili   uweze    kufuatilia    kinachoelezwa .Kwa  hiyo  
basi   kadri    unvyoendelea    kuisikiliza   ndivyo  
unavyoweza   kuielewa   vizuri 
zaidi. Kwanza  
unapoisikiliza   lugha   ikizungumza 
na   wenyewe ,  kwa   
mfano , unajifunza  MATAMSHI  SAHIHI , unajifunza    MISEMO 
ambayo  huwezi   kuipata 
katika    matukio   mengine.
     Unatakiwa
kuwa   mwangalifu  katika  
kuchagua   vipindi , kama   unachagua  
redio au  televisheni ; kuna
TAARIFA   YA   HABARI  
ambayo , hutumia  LUGHA  RASMI 
ili  uweze     KUJIFUNZA  
MANENO   YANAYOTUMIKA   KATIKA 
REJISTA  MBALIMBALI   ZA  
LUGHA.  Lakini   chagua  
vipindi   vya   DRAMA 
,  yaani   MICHEZO 
YA  KUIGIZA. Utajifunza  LUGHA  
ikizungumzwa   katika    mazingira 
yake   halisi--- NATURAL  SETTING. Matamshi , mwitiko  na 
uteuzi  wa  lugha  
unaondana   na   mazingira.SIKILIZA  VIPINDI  
VYA   DINI , SHULE , SAYANSI ,
UCHAMBUZI  na  kadhalika 
ili  uweze   kupata  
MISAMIATI   MBALIMBALI   KWA 
AJILI   YA  KUKUSAIDIA.
           HITIMISHO
----Kama 
unajifunza  LUGHA  YA 
KIGENI , fanya  marudio , mazoezi  mengi 
na  soma  vitabu 
vingi  vya   hadithi 
vya  lugha  hiyo.
-----Soma 
ukiwa  na  KAMUSI  
na   tafuta  maana 
ya  neno   usilolijua.
----Jizoeze  KUSIKILIZA 
na  KUONGEA  ukiwaiga 
wajuao  ujifunzapo  lugha  
ya  kigeni.
-----Sikiliza  MIHADHARA  
na  REDIO  ili   
ujifunze   kwa  wengine  
wanavyotamka  maneno.
-------Jikumbushe   MANENO  
magumu   kila   siku.
------Kila  
nafasi   unayoipata   itumie  
kwa    kusoma.
------Pambana  na  
SARUFI  za  LUGHA 
YA  KIGENI   kikamilifu.
------Jifunze  lugha 
ya  kigeni  kwa  
kuongea   mara   kwa 
mara.
Asante   sana  wadau 
wangu   hasa  WANAFUNZI   wangu  
kwa   kusoma  makala 
hii   nzuri   sana 
kama  utaweza   mwonyeshe 
mwenzako   naye  asome   
apate    kuelewa  jinsi  
ya   kukuza 
lugha  ya   kiingereza 
na   lugha   nyingine.
Kama  utakuwa   na   mchango  wako  wa   mawazo    karibu  sana    wadau   wangu na  wasomaji  wangu  !  ANDIKA    MAONI , USHAURI  HAPO   CHINI . 
                       MUNGU  AWABARIKI  SANA !
Makala  hii  imeandikwa 
na   MWL  
JAPHET    MASATU , DAR  ES 
SALAM , TANZANIA ,AFRIKA  YA  MASHARIKI 
anapatikana  kwa    namba    
+255 716   924 
136 ,  EMAIL:
japhetmasatu@yahoo.com
 
 











































