AN ONLINE PLATFORM THAT PROVIDES EDUCATIONAL CONTENT,SYLLABUSES, STUDY NOTES/ MATERIALS ,PAST PAPERS, QUESTIONS & ANSWERS FOR THE STUDENTS,FORM I--VI ,RESITTERS,QT, ADULT LEARNERS, COLLEGE STUDENTS, PUPILS, TEACHERS, PARENTS,TEACHERS OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA AND WORLDWIDE.YOU ARE WELCOME TO SHARE YOUR KNOWLEDGE AND IDEAS.ENJOY MASATU BLOG.YOU CAN MAKE A DIFFERENCE.YOU CAN ACHIEVE EXCELLENCE. "LEARN.REVISE.DISCUSS".Anytime, Anywhere.
- HOME
- UTAKUZAJE UWEZO WAKO WA LUGHA ?
- MBINU ZA KUSOMA NA KUFAULU MITIHANI
- HOW TO IMPROVE YOUR MEMORY
- ONLINE LEARNING & DISTANCE LEARNING ( E--LEA...
- O-LEVEL & A--LEVEL SYLLABUS
- FORM FOUR ( F 4 )--SUBJECTS---TANZANIA
- FORM TWO ( F 2 )--SUBJECTS---TANZANIA
- FORM ONE ( F 1 )-- SUBJECTS---TANZANIA
- FORM FIVE( F 5 ) AND SIX ( F 6 )--SUBJECTS ---TANZANIA
- FORM THREE ( F 3 ) SUBJECTS----TANZANIA
- STANDARD 1 & 2 SUBJECTS / MASOMO YA DARASA 1 & 2-...
- STANDARD 3 & 4 SUBJECTS / MASOMO YA DARASA 3 & 4...
- STANDARD 5, 6 & 7 SUBJECTS / MASOMO YA DARASA...
Thursday, April 30, 2020
Tuesday, April 28, 2020
Monday, April 27, 2020
FORM TWO ( F 2 )---EXAMS PAPERS--BIOLOGY, PHYSICS, CHEMISTRY, BASIC MATHEMATICS, GEOGRAPHY , HISTORY , KISWAHILI , ENGLISH, CIVICS , ARABIC LANGUAGE , ELIMU YA DINI YA KIISLAMU---MARCH--APRIL , 2020--CORONA HOLIDAY EXAMINATIONS--KINONDONI MUSLIM SECONDARY SCHOOL---DAR ES SALAAM--TANZANIA---- ( PDF )
Sunday, April 26, 2020
Thursday, April 23, 2020
Tuesday, April 21, 2020
Monday, April 20, 2020
Sunday, April 19, 2020
Friday, April 17, 2020
Monday, April 13, 2020
Sunday, April 12, 2020
Saturday, April 11, 2020
Friday, April 10, 2020
Thursday, April 9, 2020
Wednesday, April 8, 2020
Monday, April 6, 2020
UMEZALIWA ILI UFANIKIWE / YOU ARE BORN TO SUCCEED. HUFANIKIWI KWA SABABU ZIFUATAZO : --
 Mambo kumi ( 10 ) unayopenda kufanya kila siku, ambayo yanakuzua isifikie ushindi wako :--
( 1 ). HUJACHAGUA  KUWA  MSHINDI.
Hatua
 ya kwanza kuchukua ili kufikia ushindi kwenye maisha yako, ni kuchagua 
ushindi unaotaka kwenye maisha yako. Upo usemi kwamba kama hujui 
unakokwenda, njia yoyote itakuwa sahihi kwako. Hivi ndivyo wengi 
wanaendesha maisha yao, hawajui wanataka nini, ila wako bize kweli 
kweli.
Chagua leo unataka ushindi wa aina gani kwenye maisha yako ili uweze kuchukua hatua sahihi za kukufikisha kwenye ushindi huo.
 ( 2 ). HUJACHUKUA  JUKUMU  LA  MAISHA  YAKO.
Kama
 umewahi kulalamika au kumlalamikia mtu mwingine juu ya jambo lolote 
linalohusu maisha yako, basi jua unajizuia kushinda. Washindi wanachukua
 jukumu la maisha yao kwa asilimia 100. Chochote kinachotokea kwenye 
maisha yao, wanajua wa kwanza kulaumiwa na kulalamikiwa ni wao wenyewe. 
Kulalamika na kulaumu ni rahisi, lakini inakufanya ujione usiye na hatia
 na uwezo wa kupambana kwenye maisha yako.
Amua leo kushika hatamu ya maisha yako, chukua jukumu la maisha yako kwa asilimia 100 kwa kutokulalamika au kumlaumu yeyote.
(3 ). HUAMINI  KWAMBA  UNAWEZA  KUSHINDA / KUFANIKIWA.
Unapokutana
 na changamoto kidogo, unakata tamaa na kuona safari ya mafanikio 
haiwezekani. Watu wanapokupinga na kukukosoa unawasikiliza na kuona wapo
 sahihi kuliko wewe. Na hilo limekuwa kikwazo kwako. Ushindi unataka 
ujiamini kupitiliza, uamini unaweza kufanya chochote unachopanga, licha 
ya ugumu au changamoto unazopitia. Na ukweli ni kwamba, ukiamini na 
kuamua, hakuna kinachoshindikana.
Jiamini kwamba unaweza kushinda, licha ya magumu na changamoto unazopitia, endelea kuweka juhudi na utafikia ushindi mkubwa. 
( 4 ). HUNA  MALENGO  YANAYOPIMIKA.
Dhana
 yako ya malengo ni potofu, kwa sababu unajiambia tu kwamba mwaka huu 
nitafanikiwa zaidi, nitaongeza kipato, nitaanzisha biashara na 
kadhalika. Kujiambia kauli kama hizo siyo malengo, bali ni matamanio. 
Malengo ni pale unapopanga nini unataka, kwa kiwango gani na kufikia 
lini. Kama umepanga kuanza biashara, unajiambia kabisa ni biashara ya 
aina gani na utakuwa umeianza kufikia tarehe gani. Kama huwezi kupima 
malengo, huwezi kuyafikia.
Weka
 malengo yanayopimika na kila siku jipime kwa malengo hayo, gawa malengo
 hayo kwenye hatua za kuchukua na kila siku chukua hatua hizo bila 
kuacha na utafika kwenye ushindi.
 ( 5 ) . UMEKOSA   UAMINIFU.
Umekuwa
 unasikiliza kauli za wale walioshindwa, ambao wanaamini wale 
waliofanikiwa kuna namna wamefanya. Utawasikia masikini wakisema 
matajiri ni wezi na walaghai. Utawasikia wasioweka juhudi wakisema 
waliofanikiwa wana bahati. Wengine wanakuja kwako na njia za mkato za 
kufanikiwa, ambazo hazihitaji kazi yoyote. Wewe kwa kutokuijua misingi 
ya mafanikio, unaingia kwenye mitego hiyo, kinachotokea ni unajikuta 
unapoteza muda wako na hakuna hatua unazopiga.
Chagua
 kuwa mwaminifu, kufanya kile kilicho sahihi kulingana na misingi ya 
mafanikio na siyo kudanganyika au kufuata mkumbo. Njia zisizo sahihi 
zinaweza kukupa ushindi, lakini hautadumu. 
(6). HUWEKI  KAZI.
Umesikiwa
 watu wanakuambia usifanye kazi kwa nguvu, bali fanya kwa akili, wana 
kiingereza chao wanakuambia Don’t work hard, work smart. Ni uongo, 
hakuna ushindi unaopatikana bila kuweka nguvu na akili, tena kwa viwango
 vya juu sana. Watu wengi ni mashabiki na wafuatiliaji wa michezo 
mbalimbali. Nitajie mchezaji mmoja unayemkubali sana, ambaye wakati 
wenzake wanaenda kwenye mazoezi ya nguvu, yeye anafanya mazoezi kwa 
akili? Hakuna. Halafu wewe unajidanganya kwamba unaweza kufikia ushindi 
kwa akili bila nguvu!
Amua
 kuweka kazi, kazi hasa na siyo ya kitoto. Fanya kazi kwa juhudi na 
maarifa, nenda hatua ya ziada, toa thamani kubwa na ushindi utakuwa 
wako.
(7 ). HUTHAMINI  MUDA  WAKO.
Unauchukulia
 muda wako poa sana, unautawanya kama vile una chemchem ya muda isiyo 
kauka. Unapoteza muda wako wa thamani kwenye mambo yasiyo na mchango 
wowote kwenye ushindi wako, kwa sababu hujui hata thamani ya muda huo. 
Unahangaika na habari mbalimbali, umbeya, udaku, maisha ya wengine na 
mengine mengi. Halafu unakuja kulalamika kwamba huna muda wa kufanya 
zaidi yale uliyopanga kufanya.
Upe
 muda wako thamani, jua ni kiasi gani cha kipato unataka kupata, kisha 
kigawe kwa masaa na jua saa yako moja ina thamani ya shilingi ngapi. 
Hivyo unapopoteza muda, unajua kabisa ni kiasi gani cha pesa umepoteza.
 (8 ). UNASIKILIZA  SANA  HOFU  ZAKO.
Hakuna
 mtu asiyekuwa na hofu, ila wewe unazisikiliza sana hofu zako, hivyo 
huthubutu kufanya kitu chochote kipya na kikubwa, kwa sababu unahofia 
kushindwa. Wanaoshinda wanapata hofu kama zako, lakini wanajua dawa ya 
hofu ni kufanya. Kuwa na hofu ni kawaida, ila kuzisikiliza hofu zako na 
kuzifuata ni kuchagua kuukosa ushindi.
Amua leo kuchukua hatua kwenye yale unayohofia, kwa sababu ndiyo yamebeba mafanikio yako na dawa ya hofu ni kufanya unachohofia.
 ( 9 ). HUJIFUNZI  KILA  SIKU.
Unapata
 muda wakula mara tatu kwa siku, kufuatilia habari, kufuatilia maisha ya
 wengine na kulala, lakini unajiambia huna muda wa kusoma vitabu. Hapo 
ndipo unapoagana na ushindi wako. Kwa sababu hakuna mshindi ambaye 
hajifunzi kila siku. Moja ya mahitaji ya maisha ya ushindi ni kila siku 
kuwa bora kuliko siku iliyopita, na ubora pekee utaupata kupitia 
kujifunza kila siku na kufanyia kazi yale unayojifunza.
Chagua
 sasa kujifunza kila siku, haijalishi siku yako imebana kiasi gani, 
hakikisha unatenga muda wa kujifunza kupitia usomaji wa vitabu na 
mafunzo ya aina nyingine. Usikubali siku ipite hujajifunza kitu kipya.
 ( 10 ). BADALA  YA  KUZALISHA  MATOKEO , UNAZALISHA  SABABU.
Kabla
 hata hujaanza kufanya kitu, tayari umeshatengeneza sababu za kujitetea 
utakaposhindwa kwenye kitu hicho. Hivyo badala ya kuweka nguvu zako 
kubwa kuzalisha matokeo ya ushindi unayotaka, unapeleka nguvu hizo 
kuzalisha sababu za kujitetea. Huwezi kuzalisha sababu na matokeo kwa 
pamoja, chagua kuzalisha sababu na kuachana na matokeo au kuzalisha 
matokeo na kuachana na sababu.
Kataa kuwa mtu wa sababu, kuwa mtu wa kujisukuma kwa kila namna kupata matokeo unayotaka, usiwe mtu wa kukimbilia sababu.
Subscribe to:
Comments (Atom)
 
