AN ONLINE PLATFORM THAT PROVIDES EDUCATIONAL CONTENT,SYLLABUSES, STUDY NOTES/ MATERIALS ,PAST PAPERS, QUESTIONS & ANSWERS FOR THE STUDENTS,FORM I--VI ,RESITTERS,QT, ADULT LEARNERS, COLLEGE STUDENTS, PUPILS, TEACHERS, PARENTS,TEACHERS OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA AND WORLDWIDE.YOU ARE WELCOME TO SHARE YOUR KNOWLEDGE AND IDEAS.ENJOY MASATU BLOG.YOU CAN MAKE A DIFFERENCE.YOU CAN ACHIEVE EXCELLENCE. "LEARN.REVISE.DISCUSS".Anytime, Anywhere.
- HOME
- UTAKUZAJE UWEZO WAKO WA LUGHA ?
- MBINU ZA KUSOMA NA KUFAULU MITIHANI
- HOW TO IMPROVE YOUR MEMORY
- ONLINE LEARNING & DISTANCE LEARNING ( E--LEA...
- O-LEVEL & A--LEVEL SYLLABUS
- FORM FOUR ( F 4 )--SUBJECTS---TANZANIA
- FORM TWO ( F 2 )--SUBJECTS---TANZANIA
- FORM ONE ( F 1 )-- SUBJECTS---TANZANIA
- FORM FIVE( F 5 ) AND SIX ( F 6 )--SUBJECTS ---TANZANIA
- FORM THREE ( F 3 ) SUBJECTS----TANZANIA
- STANDARD 1 & 2 SUBJECTS / MASOMO YA DARASA 1 & 2-...
- STANDARD 3 & 4 SUBJECTS / MASOMO YA DARASA 3 & 4...
- STANDARD 5, 6 & 7 SUBJECTS / MASOMO YA DARASA...
Tuesday, September 8, 2015
Tuesday, September 1, 2015
Tuesday, August 25, 2015
MBINU ZA KUSOMA NA KUFAULU MITIHANI----NA MWL. JAPHET MASATU -----CALL / SMS / WHATSAP + 255 716 924 136
Kila mzazi angependelea
mwanae afanikiwe katika
masomo na kufaulu
mitihani yake. Pia
kila mwanafunzi anahitaji
KUFAULU katika mitihani
yake . Walimu nao hujisikia
vizuri wakati wanafunzi
wao wanapofanya vizuri
katika mitihani yao.
KUFAULU mtihani
ni muhimu kwa
malengo ya mwanafunzi , kwani anaposhinda
mitihani humwezesha kuwa
na mtazamo wa
juu kielimu , kwa
mfano KUPATA CHETI , DIPLOMA
AU DIGRII, kitu ambacho
humfanya afae kwenye
KAZI. Wakati mwingine inakuwa
ni vigumu kwa
baadhi ya WANAFUNZI
kumudu MASOMO na
mitihani yao. WAKATI HUO
HUO wapo baadhi
yao ambao wao
KUFAULU MITIHANI si
tatizo.
Sasa mtu
anaweza kujiuliza , kwa
nini WANAFUNZI wengine
WASHINDWE na wengine
WAFAULU vizuri katika
Masomo NA MITIHANI
yao ? MAFANIKIO katika
MASOMO na KUFAULU
MITIHANI kunahitaji UWEZO
WA ASILI , KUFANYA KAZI
KWA BIDII na
KUFUATA KANUNI NA
MBINU ZA KUSOMA.
Wanafunzi wengine
huona ugumu katika
MASOMO na KUFAULU
MITIHANI , si kwa
sababu hawana akili ,
bali hawafuati MBINU
na KANUNI fulani
za KUSOMA na
KUFAULU MITIHANI. WANAFUNZI
wengi wana uwezo
mzuri , kama watajifunza mbinu
hizi.
Mbinu na
kanuni hizi zinazweza
kutumiwa na wanafunzi
wa SHULE
ZA MSINGI , SEKONDARI ,
VYUO na hata
VYUO VIKUU.
KANUNI ZA KUSOMA
{1}. Weka LENGO maalumu
la KUSOMA kila siku
na litimize.
{2}. Jiandae kwa mtihani
kila wakati , usingoje mwalimu
atangaze kuwa ataleta
mtihani ndipo usome. SOMA
KILA SIKU.
{3}.Weka RATIBA ya
kila somo na
ifuate.
{4}.Tenga muda wa
kutosha kwa
kila somo.
{5}.Uwe na mahali
maalumu pa kusomea.
{6}.Epuka kitu chochote
kinachoweza kukufanya usisome
vizuri.
{7}.Tafuta mahali pasipo
na kelele za
aina yoyote.
{8}.Usifanye
mambo mengi kwa
wakati mmoja.Kwa mfano ,
MAPENZI au ANASA
ZA KIMWILI wakati
ungali mwanafunzi.Hivyo ni
vikwazo masomoni.
{9}.Jijengee
tabia njema ya
kujizuia katika tama
za mwili.
{10}. Fanya
MAZOEZI ya mwili mara
kwa mara.
{11}.Jiwekee
MUDA wa kutosha
kila siku kwa
ajili ya kazi
za utoaji taarifa
za MASOMO na
PROJEKTI.
{12}.Ni jambo la
busara kuwa na usiku
mmoja wa kumpumzika
katika juma ambayo
si Jumapili au
Jumamosi.
{13}.Ni muhimu kujihusisha
na watu wengine ,
jambo hili litakufariji
kimawazo.
WAKATI WA
KUJISOMEA
{14}. Kabla
hujaanza kujisomea , hakikisha
kuwa zana zote
muhimu kwa kusomea
zipo.
{15}.Epuka
vishawishi vinavyoewza kukufanya
uairishe KUJISOMEA.
{16}.Tafuta mahali pasipo
na kelele za
aina yoyote.
{17}.Hakikisha
kuwa mahali pa
kusomea pana mwanga
wa kutosha.
{18}.Usisome
mambo mengi kwa
wakati mmoja.
{19}.Epuka
kusoma hadi usiku
sana; utaharibu afya yako.
{20}.Jisomee
katika MUDA unodhani
unafaa zaidi.
{21}.Epuka
KUSOMA ukiwa umejilaza
kitandani.
{22}.Uwe na MUDA
wa KUPUMZIKA kila
unapochoka KUSOMA.
{23}.Uwe na muda
mwingi wa KUJISOMEA
kila siku , usipoteze
MUDA kwa mambo
yasiyo ya lazima
kama vile MAONGEZI.
UNAPOKUWA SHULENI /
CHUONI / DARASANI FANYA
YAFUATAYO
{24}. Fika
darasani kwa wakati
unaotakiwa ili usikose MAAGIZO.
{25}. Usikose kipindi bila
sababu maalumu.
{26}.Wakati
mwalimu hajafika darasani ,
pitia yale uliyojifunza
kipindi kilichopita.Soma kazi
zako zote za
darasani kabla ya
kuanza darasa.
{27}.Wakati Mwalimu
anafundisha darasani SIKILIZA
KWA MAKINI kile
anachofundisha na mwangalie
machoni mwalimu usiangalie pembeni .
{28}.Baada ya kipindi , pitia yale
uliyojifunza.
{29}.Chunguza
masomo yako ili ujue
udhaifu wako uko
wapi.
{30}.Jenga tabia ya
UVUMILIVU na kamwe
usikate tama wakati
ugumu unapoibuka masomoni.
{31}.Jenga tabia ya
kupania KUFAULU katika
MASOMO yako. AMINI KUWA
UTAFAULU.
{32}.Usiwe
MWANAFUNZI wa kukaa
tu darasani, ULIZA na
JIBU MASWALI yanapoulizwa.
{33}.Epuka kukaa kimya
na nyuma ya
darasa , bali shiriki
katika mazungumzo ya darasani
na wenzako.
{34}.Ni vizuri pia
kuwa na MWENZAKO
wa kujadili naye.
{35}.Uwe
MWANAFUNZI mdadisi wa
mambo kwa walimu
na hata kwa wanafunzi
wenzako pia.
{36}. Wasilisha
kazi za darasani
kwa wakati wake.
{37}.Unapokuwa na matatizo
kimasomo, mwone mwalimu , anayehusika.
{38}.Hudhuria
shughuli zote za
shule nje ya
darasani.
{39}. Jenga
uhusiano mzuri kwa
walimu wako na
kwa wanafunzi wenzako.Ukiwa na
AMANI moyoni , utasoma na
kuelewa. JISTAHI na
KUWAPENDA walimu wako. Ukimpenda mwalimu
utalielewa vzuri somo
lake.
{40}.Epuka
marafiki wabaya wenye
nia ya kukupotosha.
{41}. Epuka POMBE ,
UVUTAJI WA SIGARA , BANGI na
MADAWA YA KULEVYA.Huharibu ubongo
na kudhoofisha afya.
KABLA YA
MITIHANI FANYA HAYA
{42}.Kabla ya mtihani , SOMA KWA
BIDII SANA usingoje
mtihani umekaribia ndipo
usome.
{43}.SOMA kwa mpangilio
kila siku ili
KUJIANDAA kikamilifu kwa
MTIHANI.
{44}.USIKU unaofuatiwa na
siku ya mtihani
uwe na MUDA
WA KUTOSHA WA KULALA.
KULALA.Usisome hadi
usiku wa manane.
SIKU
YA MITIHANI FANYA
HAYA
{45}.Siku ya mtihani , usifikirie kushindwa
bali uwe na
IMANI kuwa utashinda.ONDOA WASIWASI
NA MASHAKA.
{46}.Wahi kwenye chumba
cha mtihani kwani
kuchelewa huleta HOFU.
{47}.Chukua vifaa vyote muhimu
katika mtihani kama
vile kalamu, penseli na
rula.
{48}.Soma MAAGIZO YA
MTIHANI kwa uangalifu
sana, na hakikisha
uko makii kwa
kile unchotakiwa kufanya
kabla ya kujibu
swali lolote
{49}. Kabla
hujaanza kujibu maswali , angalia maswali
ambayo ni rahisi kwako
kujibu.
{50}.JIBU maswali
rahisi kwanza na kwa
haraka ili upate
MUDA wa kutosha
kujibu maswali magumu.
Asante sana wanafunzi
wangu wa SHULE
ZA MSINGI, SEKONDARI, VYUO
na VYUO VIKUU
kwa kusoma makala
hii nzuri sana. Mwandishi
wa makala hii
ni MWL JAPHET
MASATU , anapatikana kwa CALL / SMS / WHATSAPP + 255 716 924 136 ,
EMAIL, japhetmasatu@yahoo.com , DAR ES
SALAAM, TANZANIA, AFRIKA YA
MASHARIKI.
MUNGU AWABARIKI WOTE
Sunday, August 23, 2015
UTAKUZAJE UWEZO WAKO WA LUGHA ?
MAKALA hii nimeiandika
maalumu kwa watanzania na
wadau wangu wote ,
wanafunzi wa SHULE ZA MSINGI , SEKONDARI, na VYUO wanaopenda
kujifunza LUGHA
YA KIINGEREZA na lugha
nyingne ngeni KUJIFUNZA MBINU NA KANUNI za kuikuza LUGHA hii lengo ni KUWEZA KUANDIKA
na KUONGEA kwa
UFASAHA na UMAHIRI LUGHA YA KIINGEREZA.
Limekuwa ni
tatizo kubwa kwa Watanzania wengi na wanafunzi wetu kuanzia ELIMU AWALI, MSINGI,SEKONDARI , VYUO kutoweza
kuongea KIINGEREZA
kwa ufasaha na
umahiri.Hata Lugha ya
KISWAHILI ingawa ni
lugha yetu ya
taifa bado ni
tatizo kwa watanzania
wengi na wanafunzi
kuongea kwa
ufasaha na umahiri ! TATIZO
NI NINI ? UTAKUZAJE UWEZO
WAKO WA LUGHA ? Kujifunza LUGHA yoyote
ni suala
ENDELEVU {long and permanent term
} na
siyo suala la
KUJIFUNZA LUGHA KWA
WIKI TATU TU,
AU MIEZI MITATU
TU ,AU MIEZI
SITA TU ! KAMA MATANGAZO
YA BIASHARA YANAVYOJITANGAZA . “ JIFUNZE LUGHA
YA KIINGEREZA KWA
WIKI TATU “ hii si
kweli ndugu yangu.
LUGHA ni
mtaji , inaweza
kukufanikisha mambo yako
katika maisha ! Ndugu
yangu MTANZANIA kama
wewe ni mbumbumbu
wa Lugha ya
KISWAHILI au KIINGEREZA
utachina au utakwama
katika masuala yako
yanayohitaji UMAHIRI katika
lugha hizo mbili . Kuna umuhimu
sana kwa ndugu
yangu MTANZANIA kuwa
MAHIRI katika kutumia
KISWAHILI au KIINGEREZA
kwa ufasaha na umahiri .
SIRI
ZA KUIKUZA
LUGHA YA KIINGEREZA
---Huwezi kuimiliki
lugha yoyote kama
huitumii.Mtu anaweza kujidai
kuwa kwa vile
ni mswahili na
amezaliwa katika lugha
hii basi anaijua
lugha. Hii si kweli
kabisa ndugu yangu .Kama
ingekuwa hivyo basi
wote tungeweza kutumia
na kuielewa MISAMIATI
na MISEMO yote
ambayo iko katika
lugha yako.Kwanini basi
wengine wakiitumia MISEMO
na MISAMIATI hito
wewe unatoka kappa , ni
kwa sababu huitumii.Kwa
hiyo jambo la
msingi ni kuhakikisha
kuwa unaitumia lugha.
----Kwa
wale wanaojifunza lugha
ya kigeni , jambo
la msingi ni kuhakikisha
kuwa unaitumia ili
uweze kupata uzoefu
na hatimaye kuitumia
kadri unavyotaka.
-----KUITUMIA LUGHA
MAANA YAKE NINI ?
Izungumze au itumie
katika MAANDISHI ; kama ni
lugha ngeni kwako.Kadri
unavyoendelea kuitumia katika
mazungumzo au katika
kuiandika basi unakuwa
na uwezo wa
kuielewa na utahitajika
kupata misamiati mipya.
----Hudhuria katika
mikutano na uhakikishe
unatafuta nafasi ya
kuzungumza. Unapozungumza
katika matukio kama
hayo maana yake
utapaswa kuchagua MANENO/ MISAMIATI na
kuyapanga ili uonekane
unajieleza kwa ufasaha
na kile kinachokusudiwa. UWEZO WA
LUGHA UTAHITAJIKA.
-----Makongamano , au hata
ubishi wa kawaida
mitaani ni nafasi
nzuri kwako wewe
kuitumia ili uweze
kukuza uwezo wako
wa lugha. Na wewe
uingie katika ubishi
halafu uangalie , fanya tathmini , baadaye , kwa nini
ulishindwa au kushinda, kwa nguvu
ya hoja au
kwa hoja ya
nguvu.Kama unamiliki lugha
unaweza KUSHINDA kila
KONGAMANO.
-----Jifunze kutunga
HADITHI au kuzisoma ,
KUTUNGA MASHAIRI.Haya ni
mambo pekee yanayoweza
kukufanya uhitaji uwezo
mkubwa wa lugha
na hazina kubwa
ya MISAMIATI.
UTATUNGAJE MASHAIRI
KAMA MISAMIATI YAKO
NI MICHACHE ?
Aidha ukitunga MASHAIRI
au HADITHI utajikuta
nyakati zote unatafuta
KAMUSI au VITABU
vya MISEMO na
lugha ili uweze
kupata MANENO yanayofaa
katika utunzi wako
kwa ajili hii
LUGHA yako inakua
kwa haraka sana.
Lakini zuri
sana hapa ni
kuwa kadri unavyoendelea kujihusisha
na utunzi wa
MASHAIRI au HADITHI UNATUMIA
MUDA MWINGI KUFIKIRI ,
na jinsi unavyoendelea kushughulika na
mambo hayo, uwezo wako
wa KUFIKIRI NA KUTAFAKARI
nao huongezeka. Ongezeko
la uwezo wako wa
KUFIKIRI ni matokeo
ya kuwa na
UWEZO MKUBWA WA
LUGHA.
----SIKILIZA , Wengine hudhani
KUSIKILIZA sio sehemu
ya kutumia / kujifunza LUGHA.
-----FUNGULIA REDIO, utasikiliza MISEMO
na MISAMIATI mbalimbali
ambayo utahitajika kuielewa
ili uweze kufuatilia kinachoelezwa .Kwa hiyo
basi kadri unvyoendelea kuisikiliza ndivyo
unavyoweza kuielewa vizuri
zaidi. Kwanza
unapoisikiliza lugha ikizungumza
na wenyewe , kwa
mfano , unajifunza MATAMSHI SAHIHI , unajifunza MISEMO
ambayo huwezi kuipata
katika matukio mengine.
Unatakiwa
kuwa mwangalifu katika
kuchagua vipindi , kama unachagua
redio au televisheni ; kuna
TAARIFA YA HABARI
ambayo , hutumia LUGHA RASMI
ili uweze KUJIFUNZA
MANENO YANAYOTUMIKA KATIKA
REJISTA MBALIMBALI ZA
LUGHA. Lakini chagua
vipindi vya DRAMA
, yaani MICHEZO
YA KUIGIZA. Utajifunza LUGHA
ikizungumzwa katika mazingira
yake halisi--- NATURAL SETTING. Matamshi , mwitiko na
uteuzi wa lugha
unaondana na mazingira.SIKILIZA VIPINDI
VYA DINI , SHULE , SAYANSI ,
UCHAMBUZI na kadhalika
ili uweze kupata
MISAMIATI MBALIMBALI KWA
AJILI YA KUKUSAIDIA.
HITIMISHO
----Kama
unajifunza LUGHA YA
KIGENI , fanya marudio , mazoezi mengi
na soma vitabu
vingi vya hadithi
vya lugha hiyo.
-----Soma
ukiwa na KAMUSI
na tafuta maana
ya neno usilolijua.
----Jizoeze KUSIKILIZA
na KUONGEA ukiwaiga
wajuao ujifunzapo lugha
ya kigeni.
-----Sikiliza MIHADHARA
na REDIO ili
ujifunze kwa wengine
wanavyotamka maneno.
-------Jikumbushe MANENO
magumu kila siku.
------Kila
nafasi unayoipata itumie
kwa kusoma.
------Pambana na
SARUFI za LUGHA
YA KIGENI kikamilifu.
------Jifunze lugha
ya kigeni kwa
kuongea mara kwa
mara.
Asante sana wadau
wangu hasa WANAFUNZI wangu
kwa kusoma makala
hii nzuri sana
kama utaweza mwonyeshe
mwenzako naye asome
apate kuelewa jinsi
ya kukuza
lugha ya kiingereza
na lugha nyingine.
Kama utakuwa na mchango wako wa mawazo karibu sana wadau wangu na wasomaji wangu ! ANDIKA MAONI , USHAURI HAPO CHINI .
MUNGU AWABARIKI SANA !
Makala hii imeandikwa
na MWL
JAPHET MASATU , DAR ES
SALAM , TANZANIA ,AFRIKA YA MASHARIKI
anapatikana kwa namba
+255 716 924
136 , EMAIL:
japhetmasatu@yahoo.com
Subscribe to:
Comments (Atom)






































