AN ONLINE PLATFORM THAT PROVIDES EDUCATIONAL CONTENT,SYLLABUSES, STUDY NOTES/ MATERIALS ,PAST PAPERS, QUESTIONS & ANSWERS FOR THE STUDENTS,FORM I--VI ,RESITTERS,QT, ADULT LEARNERS, COLLEGE STUDENTS, PUPILS, TEACHERS, PARENTS,TEACHERS OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA AND WORLDWIDE.YOU ARE WELCOME TO SHARE YOUR KNOWLEDGE AND IDEAS.ENJOY MASATU BLOG.YOU CAN MAKE A DIFFERENCE.YOU CAN ACHIEVE EXCELLENCE. "LEARN.REVISE.DISCUSS".Anytime, Anywhere.
AN ONLINE PLATFORM THAT PROVIDES EDUCATIONAL CONTENT,SYLLABUSES, STUDY NOTES/ MATERIALS ,PAST PAPERS, QUESTIONS & ANSWERS FOR THE STUDENTS,FORM I--VI ,RESITTERS,QT, ADULT LEARNERS, COLLEGE STUDENTS, PUPILS, TEACHERS, PARENTS,TEACHERS OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA AND WORLDWIDE.YOU ARE WELCOME TO SHARE YOUR KNOWLEDGE AND IDEAS.ENJOY MASATU BLOG.YOU CAN MAKE A DIFFERENCE.YOU CAN ACHIEVE EXCELLENCE. "LEARN.REVISE.DISCUSS".Anytime, Anywhere.
BONYEZA HAPA CHINI / CLICK HERE BELOW.
Sunday, December 29, 2019
Saturday, December 28, 2019
Thursday, December 26, 2019
Wednesday, December 25, 2019
Tuesday, December 24, 2019
Sunday, December 22, 2019
Wednesday, December 18, 2019
Tuesday, December 17, 2019
Monday, December 16, 2019
Sunday, December 15, 2019
Saturday, December 14, 2019
Friday, December 13, 2019
Thursday, December 12, 2019
Tuesday, December 10, 2019
Sunday, December 8, 2019
Saturday, December 7, 2019
Thursday, December 5, 2019
Monday, December 2, 2019
Friday, November 29, 2019
Thursday, November 28, 2019
Thursday, November 21, 2019
Friday, November 8, 2019
Tuesday, November 5, 2019
Sunday, November 3, 2019
Friday, November 1, 2019
Sunday, October 27, 2019
Wednesday, October 23, 2019
Sunday, October 20, 2019
Saturday, October 19, 2019
Friday, October 18, 2019
Thursday, October 17, 2019
Sunday, October 13, 2019
Saturday, October 12, 2019
Thursday, October 10, 2019
Tuesday, October 8, 2019
Monday, October 7, 2019
Sunday, October 6, 2019
Saturday, October 5, 2019
Friday, October 4, 2019
Thursday, October 3, 2019
Wednesday, October 2, 2019
Tuesday, October 1, 2019
Sunday, September 29, 2019
Saturday, September 28, 2019
Friday, September 27, 2019
Thursday, September 26, 2019
Wednesday, September 25, 2019
Sunday, September 22, 2019
Friday, September 20, 2019
Thursday, September 19, 2019
Wednesday, September 18, 2019
Tuesday, September 17, 2019
Monday, September 16, 2019
Sunday, September 15, 2019
Saturday, September 14, 2019
Friday, September 13, 2019
Thursday, September 12, 2019
Tuesday, September 10, 2019
Monday, September 9, 2019
MBINU ZA KUJIBU MASWALI : UCHAMBUZI NA UHAKIKI :USHAIRI, RIWAYA / HADITHI NA TAMTILIYA-----KIDATO CHA 3 & 4
Wanafunzi na watahiniwa wanapopata swali katika mitihani wanajukumu kubwa la kulielewa kablaya kulijibu.
· Swali linataka nini hasa?
· Je, kuna mambo chanya?
· Je, kuna mambo hasi? Yepi ambayo yanatakiwa kutajwa?
(a) Yale yanayoeleza kufanana kwa vipengele vilivyo katika vitu tofauti na
(b) Kutofautiana kwa mambo katika vitu hivyo viwili. Baada ya kulinganisha kama swali linavyotaka, hatua nyingine muhimu ni kuangalia ufanisi wa kazi zote/vitu vyote viwili.
KUHUSU SHAABAN ROBERT / ABOUT SHAABAN ROBERT
- Shaaban Robert is to the Swahili language what Shakespeare was to English. Acclaimed as the national poet, his publications have always been the touchstone of beauty of language, purity of spirit, and deep wisdom informed by African and Swahili culture in particular, but imbued with respect for and understanding of other cultures. Most prominent of his work is Kusadikika (To be believed), an allegorical work of an imaginary country or state in which injustices are perpetrated against all notions of justice, law and humanity. Published at the height of colonial occupation in Tanzania.
Shaaban Robert kwa lugha ya Kiswahili ni sawa na Shakespeare kwa lugha ya Kiingereza. Akikubalika kama mshairi wa taifa, vitabu vyake daima vimekuwa kipimo cha juu cha uhondo wa lugha, usafi wa nia na hekima kutokana na utamaduni hususan wa Kiafrika na Waswahili lakini pia kwa jnsi alivyoelewa na kusheshimu tamadui nyingine. Katika vitabu vyake Kusadikika ndicho maarufu kushinda vyote. Hii ni hadithi ya kiistara juu ya nchi ambako dhuluma inatawala kinyume na haki, sheria na utu. Kitabu kilichapishwa wakati ukoloni umetanda nchini Tanzania.
WASIFU WA SITI BINTI SAAD-----RIWAYA / HADITHI-----BY SHAABAN ROBERT
Sunday, September 8, 2019
Saturday, September 7, 2019
SHAIRI : LOLIONDO KWA BABU
Watu viguu na njia, Wanoenda kwa vishindo
Kiongozi wa kanisa, Siku hizi anaganga
Siku imepambazuka, Naamshwa kwa kelele
Najifunga yangu shuka, Kutazama walo mbele
Tayari washazunguka, Kwa Kasisi Ambakile
Kiongozi wa kanisa, Siku hizi anaganga
Miujiza imefika, Babu yeye keshaota
Wote mloathirika, Anzeni kujikokota
Loliondo mkifika, Mizizi inatokota
Kiongozi wa kanisa, Siku hizi anaganga
Iwapo una nafasi, Usiende mhimbili
Ondoa na wasiwasi, Loliondo kuna dili
Dawa bei ni rahisi, Kikombe ni buku mbili
Kiongozi wa kanisa, Siku hizi anaganga
Kashinda madakitari, Walosoma hadi ng’ambo
Magonjwa yote hatari, Yalokuwepo kitambo
Eti mpaka kisukari, kweli babu ana mambo
Kiongozi wa kanisa, Siku hizi anaganga
Ukimwi unatutisha, Ugonjwa kama adhabu
Waganga wamechemsha, Kutafuta matibabu
Kama mbinu zimekwisha, Kajaribuni kwa babu
Kiongozi wa kanisa, Siku hizi anaganga
Kwa babu kuna vioja, Kabla kutoa tiba
Hutangaza yake hoja, Dawa msije kuiba
Mnapata mara moja, Sio kunywa mkashiba
Kiongozi wa kanisa, Siku hizi anaganga
Wala msifanye pupa, Walokwenda ni umati
Babu dawa akikupa, Kunywa kwa kombe la bati
Usipeleke na chupa, Ukayavunja masharti
Kiongozi wa kanisa, Siku hizi anaganga
Aponya kila madhara, Hili wengi wanakiri
Pengine ni biashara, Katumia muhubiri
Kujitoa ufukara, Ajipe na utajiri
Kiongozi wa kanisa, Siku hizi anaganga
Mara bibi wa tabora, keshaibuka na yake
Kujiona ndio bora, Na yeye afaidike
Watu kweli ni wakora, Jamani tuwajibike
Kiongozi wa kanisa, Siku hizi anaganga
Sijui kama ya kweli, Msije mkasusia
Mi nahisi utapeli, Mbuzi ndani ya gunia
Dawa sijaikubali, Maajabu ya dunia?
Kiongozi wa kanisa, Siku hizi anaganga
Namefika kaditama, Dawa zinanitatiza
Babu ataniandama, Malenga kuniapiza
Ninaogopa lawama, Shairi nimemaliza
Kiongozi wa kanisa, Siku hizi anaganga
HAMZA A. MOHAMMED
Thursday, September 5, 2019
Wednesday, September 4, 2019
Sunday, September 1, 2019
Saturday, August 31, 2019
Thursday, August 29, 2019
Tuesday, August 27, 2019
Saturday, August 24, 2019
Friday, August 23, 2019
Wednesday, August 21, 2019
Tuesday, August 20, 2019
Sunday, August 18, 2019
LUGHA NA UTAMADUNI---NADHARIA YA SAPIR ---WHORF
- Lugha ni sauti za nasibu zinazotumiwa na watu katika kuwasiliana miongoni mwao.
- Jamimi ni kundi la watu wanaoishi pamoja na wenye kuhusiana kijamii, kikazi au kiuchumi na yenye kutumia lugha moja kwa ajili ya mawsiliano yao.
- Lugha imefungamana na jamii kiasi kwamba haiwezi kutenganishwa na maisha ya kijamii ya binadamu.
– Lugha ni kielelezo cha mahusiano ya kijamii yaani hueleza jinsi jamii inavyohusiana na mazingira yao halisi na namna wanajamii wanavyohusiana wenyewe kwa wenyewe.
– Lugha hubadilika kulingana na mabadiliko ya kijamii. Pamoja na uhusiano huu baina ya jamii na lugha, hakuna uhusiano wa moja kwa moja baina ya lugha na jamii kwa sababu:
i) Lugha sio lazima iwe ya watu wa jamii ile ile. Mathalani Kiswahili sio lugha ya Waswahili peke yao.
ii) Watu wanaoishi katika nchi sio lazima wawe wa asili ya nchi hiyo, kwa hivyo jina la jamii yao haiwezi kuwiana na lugha wanayoongea.
iii) Lugha moja huwa na vilugha kadha ndani mwake, mathalani lugha ya Kiingereza ina viingereza yaani lahaja kadha, mfano: Kiskochi, Kikoknii, Kilancastar n.k.
iv) Kuna jamii yenye jina tofauti na lugha wanayozungumza, mathalani Marekani hawazungumzi Kimarekani bali Kiingereza, Tanzania kuna Kiswahili na sio Kitanzania
SHAIRI : NAKUENZI KAMBARAGE
**********
Siwezi kukukumbuka,
kimya kimya mtukuka,
mwelekezi muafaka,
u wa maana hakika,
ut’endelea tajika,
milele yote milele.
****
Kwa dhati toka moyoni,
ni shahidi Maanani,
Baba ali mhisani,
wa wanyonge niamini,
alikuwa ni makini,
wa haki za binadamu.
****
Nyerere wetu shujaa,
Afrika aliifaa,
wasifa wake wajaa,
yote yote mataifaa,
mengi mema ulifanzaa,
nakuenzi Kambarage.
****
Shukurani Maanani,
kunigea tungo hini,
nikimtaja mwendani,
aliyeko mtimani,
kulla wa bora imani,
amkumbuke Nyerere.
***
Rwaka rwa Kagarama,
Mshairi Mnyarwanda.