BONYEZA HAPA CHINI / CLICK HERE BELOW.

Tuesday, August 25, 2015

MBINU ZA KUSOMA NA KUFAULU MITIHANI----NA MWL. JAPHET MASATU -----CALL / SMS / WHATSAP + 255 716 924 136



  
Kila    mzazi  angependelea  mwanae  afanikiwe   katika  masomo  na   kufaulu  mitihani  yake.  Pia  kila   mwanafunzi   anahitaji    KUFAULU   katika  mitihani    yake . Walimu  nao  hujisikia  vizuri  wakati   wanafunzi  wao   wanapofanya   vizuri   katika   mitihani  yao.
      KUFAULU   mtihani   ni  muhimu  kwa  malengo   ya   mwanafunzi , kwani    anaposhinda  mitihani   humwezesha   kuwa  na  mtazamo   wa  juu  kielimu ,  kwa  mfano   KUPATA  CHETI ,  DIPLOMA  AU  DIGRII, kitu  ambacho   humfanya  afae  kwenye   KAZI. Wakati   mwingine   inakuwa   ni  vigumu  kwa  baadhi  ya  WANAFUNZI  kumudu  MASOMO  na  mitihani  yao. WAKATI  HUO  HUO  wapo   baadhi  yao   ambao  wao   KUFAULU   MITIHANI  si   tatizo.
     Sasa   mtu  anaweza   kujiuliza ,  kwa  nini  WANAFUNZI   wengine   WASHINDWE   na   wengine  WAFAULU  vizuri  katika  Masomo  NA  MITIHANI  yao ?  MAFANIKIO  katika   MASOMO  na  KUFAULU  MITIHANI    kunahitaji  UWEZO  WA  ASILI , KUFANYA   KAZI  KWA  BIDII   na  KUFUATA   KANUNI   NA  MBINU  ZA   KUSOMA.
   Wanafunzi  wengine  huona   ugumu  katika  MASOMO  na  KUFAULU  MITIHANI ,  si  kwa  sababu  hawana  akili ,  bali  hawafuati   MBINU  na  KANUNI  fulani   za  KUSOMA  na  KUFAULU   MITIHANI.  WANAFUNZI   wengi   wana  uwezo   mzuri , kama   watajifunza   mbinu  hizi.
     Mbinu    na   kanuni   hizi  zinazweza   kutumiwa   na  wanafunzi  wa  SHULE  ZA   MSINGI ,  SEKONDARI ,  VYUO   na    hata   VYUO   VIKUU.

 KANUNI  ZA   KUSOMA
{1}. Weka  LENGO   maalumu  la KUSOMA   kila  siku  na   litimize.
{2}. Jiandae  kwa  mtihani  kila  wakati , usingoje  mwalimu    atangaze  kuwa  ataleta  mtihani  ndipo  usome. SOMA   KILA   SIKU.
{3}.Weka  RATIBA  ya  kila   somo   na  ifuate.
{4}.Tenga  muda  wa  kutosha   kwa  kila  somo.
{5}.Uwe  na  mahali  maalumu  pa  kusomea.
{6}.Epuka  kitu  chochote  kinachoweza  kukufanya  usisome   vizuri.
{7}.Tafuta  mahali  pasipo  na  kelele  za  aina   yoyote.
{8}.Usifanye  mambo   mengi   kwa   wakati   mmoja.Kwa  mfano ,  MAPENZI  au  ANASA   ZA   KIMWILI  wakati  ungali  mwanafunzi.Hivyo   ni  vikwazo  masomoni.
{9}.Jijengee  tabia   njema  ya  kujizuia  katika  tama  za  mwili.
{10}. Fanya   MAZOEZI  ya mwili  mara   kwa  mara.
{11}.Jiwekee   MUDA   wa  kutosha  kila  siku  kwa  ajili   ya   kazi   za   utoaji  taarifa  za   MASOMO   na  PROJEKTI.
{12}.Ni   jambo   la  busara  kuwa  na usiku  mmoja  wa  kumpumzika  katika   juma  ambayo  si   Jumapili  au   Jumamosi.
{13}.Ni  muhimu   kujihusisha  na  watu  wengine ,  jambo  hili   litakufariji  kimawazo.


WAKATI   WA  KUJISOMEA
{14}. Kabla  hujaanza  kujisomea ,  hakikisha  kuwa   zana  zote   muhimu  kwa  kusomea  zipo.
{15}.Epuka  vishawishi  vinavyoewza  kukufanya  uairishe  KUJISOMEA.
{16}.Tafuta  mahali  pasipo  na  kelele  za  aina   yoyote.
{17}.Hakikisha   kuwa    mahali    pa  kusomea   pana   mwanga  wa  kutosha.
{18}.Usisome   mambo  mengi   kwa   wakati   mmoja.
{19}.Epuka   kusoma   hadi  usiku   sana; utaharibu   afya   yako.
{20}.Jisomee  katika   MUDA   unodhani  unafaa  zaidi.
{21}.Epuka   KUSOMA    ukiwa  umejilaza  kitandani.
{22}.Uwe  na  MUDA  wa   KUPUMZIKA  kila   unapochoka   KUSOMA.
{23}.Uwe   na   muda  mwingi   wa  KUJISOMEA  kila   siku ,  usipoteze  MUDA  kwa  mambo  yasiyo  ya  lazima  kama  vile   MAONGEZI.


UNAPOKUWA   SHULENI /  CHUONI /  DARASANI  FANYA  YAFUATAYO
{24}. Fika   darasani  kwa  wakati  unaotakiwa  ili  usikose MAAGIZO.
{25}. Usikose  kipindi  bila  sababu   maalumu.
{26}.Wakati  mwalimu   hajafika  darasani ,  pitia  yale  uliyojifunza  kipindi   kilichopita.Soma  kazi   zako  zote  za  darasani  kabla  ya  kuanza   darasa.
{27}.Wakati  Mwalimu anafundisha   darasani    SIKILIZA  KWA  MAKINI  kile   anachofundisha  na  mwangalie   machoni  mwalimu  usiangalie pembeni .
{28}.Baada  ya  kipindi , pitia  yale  uliyojifunza.
{29}.Chunguza  masomo   yako  ili ujue  udhaifu  wako   uko  wapi.
{30}.Jenga  tabia    ya  UVUMILIVU  na  kamwe  usikate  tama  wakati  ugumu   unapoibuka   masomoni.
{31}.Jenga  tabia  ya   kupania  KUFAULU  katika  MASOMO  yako. AMINI  KUWA  UTAFAULU.
{32}.Usiwe  MWANAFUNZI  wa  kukaa   tu darasani,  ULIZA  na  JIBU  MASWALI  yanapoulizwa.
{33}.Epuka  kukaa   kimya  na  nyuma  ya  darasa ,  bali   shiriki  katika   mazungumzo   ya  darasani  na  wenzako.
{34}.Ni  vizuri  pia   kuwa   na   MWENZAKO  wa   kujadili  naye.
{35}.Uwe   MWANAFUNZI  mdadisi  wa   mambo  kwa  walimu  na hata  kwa  wanafunzi  wenzako   pia.

{36}. Wasilisha  kazi   za  darasani   kwa  wakati   wake.
{37}.Unapokuwa  na  matatizo   kimasomo, mwone   mwalimu   , anayehusika.
{38}.Hudhuria  shughuli  zote  za  shule  nje  ya  darasani.
{39}. Jenga  uhusiano  mzuri  kwa  walimu  wako  na  kwa  wanafunzi   wenzako.Ukiwa  na  AMANI   moyoni , utasoma  na  kuelewa.  JISTAHI   na  KUWAPENDA  walimu  wako. Ukimpenda  mwalimu  utalielewa   vzuri   somo  lake.
{40}.Epuka  marafiki  wabaya  wenye  nia  ya  kukupotosha.
{41}. Epuka  POMBE , UVUTAJI  WA  SIGARA , BANGI  na   MADAWA   YA KULEVYA.Huharibu  ubongo  na  kudhoofisha  afya.

KABLA    YA  MITIHANI     FANYA  HAYA
{42}.Kabla  ya   mtihani , SOMA   KWA  BIDII  SANA  usingoje  mtihani  umekaribia  ndipo  usome.
{43}.SOMA  kwa   mpangilio  kila  siku  ili    KUJIANDAA   kikamilifu  kwa      MTIHANI.
{44}.USIKU  unaofuatiwa   na   siku  ya    mtihani  uwe  na  MUDA  WA  KUTOSHA  WA  KULALA.
  KULALA.Usisome  hadi  usiku    wa  manane.

 SIKU   YA  MITIHANI   FANYA  HAYA
{45}.Siku  ya  mtihani , usifikirie   kushindwa   bali  uwe  na   IMANI  kuwa  utashinda.ONDOA  WASIWASI  NA  MASHAKA.
{46}.Wahi  kwenye  chumba  cha  mtihani  kwani  kuchelewa  huleta  HOFU.
{47}.Chukua  vifaa  vyote muhimu  katika  mtihani  kama  vile  kalamu, penseli  na  rula.
{48}.Soma  MAAGIZO  YA  MTIHANI  kwa   uangalifu  sana,  na  hakikisha  uko  makii  kwa  kile  unchotakiwa   kufanya   kabla  ya  kujibu  swali  lolote
{49}. Kabla  hujaanza  kujibu  maswali , angalia  maswali  ambayo  ni rahisi  kwako  kujibu.
{50}.JIBU   maswali   rahisi  kwanza  na kwa  haraka  ili  upate   MUDA  wa   kutosha  kujibu maswali  magumu.


Asante   sana   wanafunzi  wangu  wa  SHULE  ZA  MSINGI, SEKONDARI,   VYUO  na  VYUO  VIKUU  kwa   kusoma   makala  hii  nzuri sana.  Mwandishi  wa  makala  hii  ni   MWL  JAPHET   MASATU ,  anapatikana  kwa   CALL /  SMS /  WHATSAPP   + 255 716  924  136 ,  EMAIL,  japhetmasatu@yahoo.com ,   DAR  ES   SALAAM, TANZANIA, AFRIKA  YA MASHARIKI.
                                             
                                 MUNGU  AWABARIKI     WOTE

Sunday, August 23, 2015

UTAKUZAJE UWEZO WAKO WA LUGHA ?



MAKALA   hii   nimeiandika  maalumu  kwa  watanzania na  wadau  wangu   wote , wanafunzi wa SHULE  ZA  MSINGI , SEKONDARI,  na   VYUO  wanaopenda    kujifunza  LUGHA  YA  KIINGEREZA  na lugha  nyingne  ngeni  KUJIFUNZA   MBINU NA  KANUNI   za   kuikuza  LUGHA   hii lengo  ni  KUWEZA   KUANDIKA  na  KUONGEA  kwa  UFASAHA  na  UMAHIRI   LUGHA  YA  KIINGEREZA. 
       Limekuwa  ni  tatizo  kubwa kwa  Watanzania wengi na  wanafunzi wetu kuanzia  ELIMU AWALI, MSINGI,SEKONDARI , VYUO  kutoweza    kuongea  KIINGEREZA  kwa  ufasaha   na  umahiri.Hata   Lugha  ya  KISWAHILI  ingawa   ni  lugha   yetu  ya  taifa   bado  ni  tatizo  kwa  watanzania  wengi  na  wanafunzi   kuongea   kwa  ufasaha na  umahiri !  TATIZO  NI  NINI ? UTAKUZAJE  UWEZO   WAKO  WA  LUGHA ? Kujifunza  LUGHA  yoyote   ni   suala   ENDELEVU {long and permanent  term }  na  siyo   suala  la  KUJIFUNZA  LUGHA  KWA  WIKI  TATU  TU,  AU    MIEZI  MITATU  TU  ,AU   MIEZI   SITA  TU ! KAMA  MATANGAZO  YA  BIASHARA   YANAVYOJITANGAZA . “ JIFUNZE  LUGHA   YA  KIINGEREZA   KWA  WIKI  TATU “ hii   si   kweli    ndugu   yangu.
          LUGHA  ni  mtaji , inaweza   kukufanikisha  mambo   yako   katika  maisha !  Ndugu  yangu  MTANZANIA  kama   wewe  ni  mbumbumbu  wa  Lugha   ya   KISWAHILI  au   KIINGEREZA  utachina   au  utakwama   katika   masuala    yako   yanayohitaji  UMAHIRI  katika   lugha   hizo   mbili . Kuna   umuhimu   sana   kwa   ndugu   yangu  MTANZANIA  kuwa  MAHIRI  katika  kutumia   KISWAHILI  au  KIINGEREZA  kwa  ufasaha na  umahiri .

      SIRI    ZA   KUIKUZA    LUGHA  YA  KIINGEREZA
---Huwezi  kuimiliki  lugha  yoyote  kama  huitumii.Mtu  anaweza  kujidai  kuwa  kwa   vile  ni   mswahili   na   amezaliwa  katika   lugha   hii  basi   anaijua  lugha. Hii  si  kweli   kabisa   ndugu  yangu .Kama   ingekuwa  hivyo  basi   wote   tungeweza  kutumia  na  kuielewa   MISAMIATI  na   MISEMO  yote   ambayo  iko  katika  lugha  yako.Kwanini  basi   wengine   wakiitumia   MISEMO   na   MISAMIATI  hito    wewe  unatoka   kappa , ni  kwa  sababu  huitumii.Kwa  hiyo   jambo  la   msingi  ni  kuhakikisha   kuwa   unaitumia  lugha.
----Kwa  wale   wanaojifunza  lugha  ya  kigeni ,  jambo  la  msingi  ni  kuhakikisha  kuwa  unaitumia  ili  uweze  kupata  uzoefu   na  hatimaye  kuitumia  kadri   unavyotaka.

-----KUITUMIA  LUGHA  MAANA   YAKE   NINI ?  Izungumze  au  itumie  katika  MAANDISHI ; kama   ni  lugha   ngeni  kwako.Kadri   unavyoendelea  kuitumia  katika  mazungumzo  au   katika  kuiandika  basi   unakuwa  na  uwezo  wa   kuielewa  na   utahitajika   kupata   misamiati  mipya.
----Hudhuria  katika  mikutano  na  uhakikishe   unatafuta   nafasi  ya   kuzungumza. Unapozungumza  katika   matukio   kama  hayo   maana  yake   utapaswa   kuchagua   MANENO/ MISAMIATI  na   kuyapanga  ili  uonekane   unajieleza  kwa  ufasaha   na   kile   kinachokusudiwa. UWEZO  WA   LUGHA  UTAHITAJIKA.
-----Makongamano , au  hata  ubishi   wa  kawaida   mitaani  ni  nafasi  nzuri  kwako   wewe   kuitumia  ili   uweze   kukuza  uwezo  wako  wa  lugha. Na   wewe   uingie  katika  ubishi  halafu   uangalie , fanya  tathmini , baadaye , kwa   nini   ulishindwa   au  kushinda, kwa   nguvu  ya   hoja   au  kwa   hoja  ya   nguvu.Kama  unamiliki   lugha  unaweza    KUSHINDA   kila  KONGAMANO.
-----Jifunze  kutunga   HADITHI  au  kuzisoma ,  KUTUNGA  MASHAIRI.Haya  ni  mambo   pekee   yanayoweza  kukufanya   uhitaji   uwezo  mkubwa  wa   lugha  na  hazina  kubwa   ya   MISAMIATI.


UTATUNGAJE   MASHAIRI    KAMA   MISAMIATI   YAKO   NI  MICHACHE ?
Aidha  ukitunga   MASHAIRI  au  HADITHI   utajikuta   nyakati  zote   unatafuta   KAMUSI  au   VITABU   vya   MISEMO   na  lugha   ili   uweze  kupata  MANENO   yanayofaa  katika   utunzi  wako  kwa  ajili  hii   LUGHA  yako  inakua   kwa  haraka  sana.
     Lakini  zuri   sana   hapa   ni  kuwa  kadri    unavyoendelea   kujihusisha  na  utunzi  wa   MASHAIRI  au  HADITHI   UNATUMIA  MUDA   MWINGI  KUFIKIRI ,  na  jinsi   unavyoendelea   kushughulika   na  mambo  hayo, uwezo  wako  wa   KUFIKIRI  NA KUTAFAKARI  nao  huongezeka.  Ongezeko   la  uwezo wako   wa   KUFIKIRI  ni   matokeo   ya  kuwa   na   UWEZO   MKUBWA   WA  LUGHA.
----SIKILIZA , Wengine   hudhani   KUSIKILIZA  sio  sehemu   ya  kutumia /  kujifunza LUGHA.
-----FUNGULIA   REDIO, utasikiliza  MISEMO   na  MISAMIATI  mbalimbali    ambayo     utahitajika  kuielewa  ili   uweze    kufuatilia    kinachoelezwa .Kwa  hiyo   basi   kadri    unvyoendelea    kuisikiliza   ndivyo   unavyoweza   kuielewa   vizuri  zaidi. Kwanza   unapoisikiliza   lugha   ikizungumza  na   wenyewe ,  kwa    mfano , unajifunza  MATAMSHI  SAHIHI , unajifunza    MISEMO  ambayo  huwezi   kuipata  katika    matukio   mengine.
     Unatakiwa kuwa   mwangalifu  katika   kuchagua   vipindi , kama   unachagua   redio au  televisheni ; kuna TAARIFA   YA   HABARI   ambayo , hutumia  LUGHA  RASMI  ili  uweze     KUJIFUNZA   MANENO   YANAYOTUMIKA   KATIKA  REJISTA  MBALIMBALI   ZA   LUGHA.  Lakini   chagua   vipindi   vya   DRAMA  ,  yaani   MICHEZO  YA  KUIGIZA. Utajifunza  LUGHA   ikizungumzwa   katika    mazingira  yake   halisi--- NATURAL  SETTING. Matamshi , mwitiko  na  uteuzi  wa  lugha   unaondana   na   mazingira.SIKILIZA  VIPINDI   VYA   DINI , SHULE , SAYANSI , UCHAMBUZI  na  kadhalika  ili  uweze   kupata   MISAMIATI   MBALIMBALI   KWA  AJILI   YA  KUKUSAIDIA.

           HITIMISHO
----Kama  unajifunza  LUGHA  YA  KIGENI , fanya  marudio , mazoezi  mengi  na  soma  vitabu  vingi  vya   hadithi  vya  lugha  hiyo.
-----Soma  ukiwa  na  KAMUSI   na   tafuta  maana  ya  neno   usilolijua.
----Jizoeze  KUSIKILIZA  na  KUONGEA  ukiwaiga  wajuao  ujifunzapo  lugha   ya  kigeni.
-----Sikiliza  MIHADHARA   na  REDIO  ili    ujifunze   kwa  wengine   wanavyotamka  maneno.
-------Jikumbushe   MANENO   magumu   kila   siku.
------Kila   nafasi   unayoipata   itumie   kwa    kusoma.
------Pambana  na   SARUFI  za  LUGHA  YA  KIGENI   kikamilifu.
------Jifunze  lugha  ya  kigeni  kwa   kuongea   mara   kwa  mara.

Asante   sana  wadau  wangu   hasa  WANAFUNZI   wangu   kwa   kusoma  makala  hii   nzuri   sana  kama  utaweza   mwonyeshe  mwenzako   naye  asome    apate    kuelewa  jinsi   ya   kukuza  lugha  ya   kiingereza  na   lugha   nyingine.

Kama  utakuwa   na   mchango  wako  wa   mawazo    karibu  sana    wadau   wangu na  wasomaji  wangu  !  ANDIKA    MAONI , USHAURI  HAPO   CHINI .
                 
                       MUNGU  AWABARIKI  SANA !



Makala  hii  imeandikwa  na   MWL   JAPHET    MASATU , DAR  ES  SALAM , TANZANIA ,AFRIKA  YA  MASHARIKI  anapatikana  kwa    namba     +255 716   924  136 ,  EMAIL: japhetmasatu@yahoo.com