FASIHI  SIMULIZI. 
 
| FASIHI SIMULIZI | 
| Utanzu wa | Fasihi | 
| Kiingereza | Oral Literature | 
| Tanzu za Fasihi Simulizi |  | 
| 
 | 
| Prev | Tamathali za Usemi | 
| Next | Fasihi Andishi | 
| VIPERA VYA TANZU ZA FASIHI SIMULIZI | 
| HADITHI / NGANO |  | 
| NYIMBO | 
 Mashairi Kimai Wawe/Hodiya Nyimbo za Ndoa Nyimbo za Kidini Nyimbo za Kisiasa Za Tohara/Jandoni Nyimbo za Kizalendo | 
| TUNGO FUPI |  | 
| MAIGIZO |  | 
 
Fasihi Simulizi ni utanzu wa fasihi ambao unawakilisha sanaa ya lugha
 inayopitishwa kutoka kwa kizazi hadi kizazi kwa njia ya 
maneno/masimulizi ya mdomo.
Sifa za Fasihi Simulizi
- Hupitishwa kwa njia ya mdomo
- Ufanisi wa sanaa katika fasihi simulizi hutegemea uwezo wa msimulizi, au wahusika
- Masimulizi yake yanaweza kuathiriwa na mazingira, hisia na hali
- Ni mali ya jamii. Hakuna mtu fulani anayemiliki sanaa katika fasihi simulizi.
- Inaweza kubadilika kutoka kizazi hadi kizazi, au mazingira mbalimbali kwa sababu hutegemea kumbukumbu ya msimulizi.
- Aghalabu huwa na funzo fulani
Umuhimu wa Fasihi Simulizi
- Kuburudisha - Hufurahisha na kuchangamsha hadhira
- Kunasihi- kutolea mawaidha na kuonyesha mwelekeo unaotarajiwa katika jamii
- Kuelimisha watu kuhusu vitu mbalimbali hasa mazingira yao
- Kutambulisha jamii - jamii mbalimbali husifika kutokana na sanaa zao katika fasihi simulizi kama vile nyimbo
- Kuhifadhi na kudumisha utamaduni wa jamii
- Kuunganisha watu - huleta watu pamoja
- Kukuza lugha - fasihi huimarisha lugha kwa kuwa hutumia mbinu mbalimbali za lugha.
- Kuliwaza - hutoa huzuni na kuleta matumaini.
- Kupitisha muda - wakati mwingine fasihi simulizi hutumika kupitisha muda.
 
FASIHI  KWA  UJUMLA.
FASIHI
Katika
 uga wa fasihi kuna kumbo tatu muhimu zinazoipa uhai taaluma nzima ya 
fasihi. Kumbo hizo ni ushairi, riwaya na tamthiliya. Uwe ukweli ama 
kinyume chake lakini jambo la muhimu kufahamu ni kuwa kila kumbo katika 
fasihiutawaliwa na kanuni zake na nijambo la kiuungwana kuzifuata kanuni
 au Jadi husika. Kanuni hizo hutoa muongozo katika utungaji wa kazi za 
kifasihi na uhakiki wa kazi hizo. Aghalabu kuzitumia kanuni huwa ni 
jambo la Kiuugwana na la kheri, lakini katika zama tulizonazo sasa sio 
dhambi kubwa ya kiuandishi ahesabiwayo mwandishi na wanamapokeo 
anapokiuka jadi husika katika kumbo mojawapo ya fasihi andishi.
Tunapozungumzia
 kanuni ama Jadi ya kiutunzi katika uga wa fasihi tunamaana ya mambo 
yajitokezayo na kurudiwarudiwa mara kwa mara katika kumbo fulani ya 
fasihi, kwa mfano, mambo yajitokezayo mara kwa mara katika kumbo ya 
tamthiliya ni utumizi wa jukwaa, hadhira, wahusika, mtiririko wa 
vitendo, dhamira na nyimbo. Kama wasemavyo waswahili “Kawaida ni kama 
Sheria”, ndivyo hivyo mambo hayayanayojirudia katika kila kazi ya 
kitamthiliya ndiyo yajengayo kanuni ama sheria za utungaji wa 
tamthiliya.
Hapo
 mwanzo kabla ya kuibuka kwa fasihi ya Kiswahili ya majaribio, kanuni 
zote za ujenzi wa tamthiliya ya Kiswahili zilikopwa kutoka katika 
tamthiliya ya Ulaya. Vyanzo vingi vya taarifa vinaeleza kuwa kanuni hizi
 za ujenzi wa tamthiliya ziliwekwa na wanataaluma wa kimagharibi lakini 
ukweli ni kwamba chimbuko la tamthiliya katika nchi na tamaduni 
mbalimbali hushabihiana kwa kiasi kikubwa kwa vile uhusishwa na visakale
 na matendo ya kidini. Kwa mfano, yasemekana kuwa huko Ulaya tamthiliya 
ilitokana na miviga na viviga, hasa ya kidini, katika jamii ya kale ya 
Wayunani, (Holman 1972, katika Mulokozi1996). Miviga hiyo iliambatana na
 duru za kuzaliwa, kukua, kufa, kuoza na kuzaliwa upya ambazo hasa 
zilihusishwa na Mungu aliyeitwa Dionizi, aliyeaminiwa kuwa aliuawa, 
akakatwakatwa vipandevipande na baadaye akafufuka tena (Mulokozi 1996). 
Pia hapa Afrika, kumbukumbu za kwanza za maigizo ya kitamthiliya 
tunazipata Misri, ambako michezo ya miviga ilihusu kufa na kufufuka kwa 
Mungu wa Wamisri aliyeitwa Osiris ilikuwa ikiigizwa kila mwaka kwa miaka
 2000 kuanzia kama mwaka 2500KM, (Mulokozi 1996). Hii inaonyesha kuwa 
chimbuko la tamthiliya katika jamii nyingi duniani linashabihiana kwa 
kiasi kikubwa.  
Kanuni
 zilizowekwa juu ya ujenzi wa tamthiliya zilitokana na mambo 
yaliyopelekeachimbuko la tamthiliya. Inaonekana wazi kuwa kanuni hizi 
zilihusika na zinaendelea kuhusika kwa kiasi kikubwa katika kujenga 
muktadha, fani na vitendo vitendekavyo katika matambiko na mikusanyiko 
ya kidini, kanuni hizo kama vile utumizi wa jukwaa, hadhira, wahusika, 
vitendo, dhamira na nyimbo zinahusika moja kwa moja katika matendo 
yatendekayo katika matambiko, miviga na dini za kijadi na zile za 
kigeni.
Kanuni
 huwa hazibakii hivyohivyo, hubadilika kufuatana na mahitaji ya jamii 
kwa wakati fulani. Hapo mwanzo kanuni za Ki-Aristotle zilitumika vizuri 
na kwa usahihi katika utanzu wa tamthiliya ya kiswahili. Kadri siku 
zilivyoenda mbele watunzi wa tamthiliya ya Kiswahili walilazimika 
kukiuka baadhi ya kanuni hizo kwa kuingiza vipengele vya fasihi simulizi
 katika tamthiliya ya kiswahili ili kuifanya tasnia ya tamthiliya 
andishi ifungamane na uhalisi wa kiafrika. Waandishi wengi wa tamthiliya
 tulionao sasa ni wafuasi wazuri wa kukiuka kaida za Ki-Aristotle, ndipo
 sasa tunaona umuhimu mkubwa wa utafii huu. Vile vile ikumbukwe kuwa 
uandishi huu wa “Kimajiribio”au
 ukiukwaji huu wa kaida za kiuandishi umejitokeza katika kumbo zote za 
fasihi andishi, lakini utafiti huu umeshughulikia kumbo ya tamthiliyatu.
Ukiukwaji
 wa kaida za Ki-Aristotle na kuingizwa kwa kanuni za U-jadi (wataalamu 
wengine wanazitambulisha kanuni za U-Jadi kama fasihi ya kiswahili ya 
majaribio), katika uandishi wa tamthiliyaya Kiswahili umeibua maswali 
mengi kwa wadau wa fasihi. 
F.E.M.KSenkoro(2011:62)
 anajadili baadhi ya maswali hayo, hapa anasema “Swali ambalo hatimaye 
linajadiliwa ni; je, majaribio haya yanafuata kanuni zipi? Upya una 
nafasi gani katika majaribio? Na, Je, majaribio mahsusi ya fasihi fulani
 yanaanza na kuisha wakati gani?
Senkorohajatoa
 ufafanuzi wakutosha juu ya maswali haya. Mambo mengi ameyaacha hewani. 
Utafiti huu umeibuka na majibu kwa baadhi ya maswali na kuyaacha mambo 
mengine kama mada za utafiti kwa watafiti tarajali.
Kuna
 tafiti kadhaa zilizofanywa na kuhifadhiwa zinazohusu tamthiliya ya 
Kiswahili, tafiti nyingi kati ya hizi zinahusu uchambuzi wa vipengele 
vya fani na maudhui ndani ya tamthiliya teule. Hata hivyo kwa upeo wa 
ufahamu wa mtafiti hakuna mtafiti aliyewahi kujishughulisha kuhusu 
mabadiliko ya uandishi wa tamthiliya ya Kiswahili kutoka U-Aristotle 
kwenda U-Jadi wa Kiafrika. Wapo watafiti ambao wamefanya utafiti kuhusu 
tamthiliya kwa kuchambua vipengele mahususi,baadhi ya watafiti hao ni 
Omary (2011), alichunguza suala la Ukimwi lilivyo jadiliwa katika 
tamthiliya za Kiswahili, Murusuri (2011), alitazama Utamthiliya katika 
Ngonjera, data mahsusi alizitoka ndani ya vitabu vya Ngojera za Ukuta, 
Ngojera hizi zimetungwa na mwasisi wa chama cha UKUTA na mshairi 
mashuhuri Mathius Mnyampala. Vielevile, Madembwe (2011), alifanya 
utafiti juu ya nafasi ya kejeli na dhihaka katika tamthiliya za Penina 
Muhando. Kwa upeo wa ufahamu wa mtafiti wa utafiti huu ni kwamba hakuna 
mtafiti aliyewahi kuchunguza juu ya mabadiliko ya kiuandishi 
yaliyojitokeza katika tamthiliya ya Kiswahili kutoka uandishi unaofuata 
kanuni za Ki-Aristotle kwenda katika uandishi wenye kuzingatia vipengele
 vya Jadi ya Ki-Afrika. Kwa upeo wa mtafiti wa utafiti huu, mtafiti 
mmoja tu ndiye aliyejaribu kujadili baadhi ya matendo ya kiafrika ndani 
ya tamthiliya ya Kiswahili. Mtafiti Nicholaus, A, alichunguza jinsi 
falsafa ya Ubuntu inavyo jadiliwa katika tamthiliya ya Kiswahili.
Nicholaus
 (2011), aliteuwa tamthiliya za Penina Muhando na kuchunguza jinsi 
falsafa ya Ubuntu ilivyosawiri katika tamthiliya hizo. Malengo yake ya 
kufanya utafiti yalikuwa ni pamoja na kuelezea mbinu alizozitumia 
mwandishi Penina Muhando katika kueleza masuala ya waafrika ikiwemo na 
falsafa yao.
Katika kutekeleza lengo hilo mtafiti alitumia tamthiliya tatu za Mama Muhando, tamthiliya hizo ni Hatia, Heshima Yangu naTambueni Haki Zetu. Matokeo
 ya utafiti huu yanaonyesha kuwa falsafa ya Ubuntu imejitokea kwa kiasi 
kikubwa katika tamthiliya za Penina Muhando. Masuala ya waafrika 
yamewasilishwa kwa njia mbalimbali kama vile Ngoma, kicheko, kilio, 
kiapo, mizimu na kwa kupitia njia ya uundaji wa chama cha ZETU, kwa 
kutumia njia hizi mtafiti anayataja mambo ya waafrika yaliyojitokeza 
zaidi ndani ya tamthiliya teule kuwa ni pamoja na ndoa za kiafrika, 
burudani, hekima, upendo, heshima, ushirikiano na kadhalika. 
Pamoja
 na mtafiti kufanikiwa kuonesha mambo kadhaa yanayowahusu waafrika ndani
 yatamthiliya teule lakini hakuweza kuyaelezea mabadiliko ya kiuandishi 
katika tamthiliya ya Kiswahili. Hakutuonesha sababu zilizopeleke 
waandishi wengi wa tamthiliya ya Kiswahili kukiuka kaida za uandishi wa 
Ki-Aristotle na kuzama katika Ujadi wa Ki-Afrika, hivyo kulikuwa na haja
 ya kufanya  utafiti
 kama huu unaohusu mabadiliko ya uandishi wa tamthiliya ya Kiswahili ili
 kupata data na taarifa sahihi na za kutosha ili zitumike katika uwanja 
wa fasihi andishi. 
Mbali
 na hayo, Nicholaus alifanya Utafiti wake kwa kuchambua kazi za 
mwandishi mmoja wa tamthiliya ambaye ni Penina Muhando. Utafiti huu 
uliona ni vema kuchambua kazi za waandishi wawili ambao kwa hakika 
wanamchango mkubwa katika kustawi kwa tasnia ya tamthiliya andishi ya 
Kiswahili. Utafiti huu umechambua kazi za Ebrahim Hussein na Penina 
Muhando jambo lililomwezesha mtafiti kuongeza mawanda ya kiuchambuzi na 
ukusanyaji wa data katika kukamilisha utafiti huu. Pia uteuzi wa vitabu 
vilivyo chambuliwa na kupelekea upatikanaji wa data za msingi, ni 
tofauti na uteuzi uliofanywa na watafiti wengine kwakuwa utafiti huu 
umezingatia vipindi viwili muhimu katika uandishi wa tamthiliya, kipindi
 cha utawala wa kanuni za Ki-Aristotle na kipindi cha pili ni hiki 
tulichonacho sasa (kipindi cha fasihi ya Kiswahili ya kimajaribio).